WELCOME TO TANZANIA NATIONAL ASSEMBLY OFFICIAL BLOG: CONTACT US: P.O.BOX 941 DODOMA, TANZANIA, WEBSITE: parliament.go.tz , FIND US ON FACEBOOK >>> www.facebook.com/bungetz1, FOLLOW US ON TWITTER >>> @bunge_tz.>>>KARIBUNI

Tuesday, April 8, 2025

NAIBU SPIKA ZUNGU AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA UONGOZI BUNGENI JIJINI DODOMA












Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mussa Azzan Zungu (Mb), amengoza kikao cha Kamati ya Uongozi kilichofanyika leo tarehe 8 Aprili, 2025 katika Ukumbi wa Spika, Bungeni Jijini Dodoma.

Pamoja na mambo mengi kikao hicho kilipokea na kujadili Mapendekezo ya Ratiba ya Mkutano wa Kumi na Tisa wa Bunge.

Mkutano wa Kumi na Tisa wa Bunge umeanza leo tarehe 8 Aprili, 2025, Bungeni Jijini Dodoma.

Vile vile, Kikao hicho kilihudhuriwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu; Sera, Bunge na Uratibu, Mhe. William Lukuvi (Mb) na Katibu wa Bunge, Ndg. Baraka Leonard.