WELCOME TO TANZANIA NATIONAL ASSEMBLY OFFICIAL BLOG: CONTACT US: P.O.BOX 941 DODOMA, TANZANIA, WEBSITE: parliament.go.tz , FIND US ON FACEBOOK >>> www.facebook.com/bungetz1, FOLLOW US ON TWITTER >>> @bunge_tz.>>>KARIBUNI

Monday, February 28, 2022

SPIKA DKT. TULIA NA MBUNGE WA MBEYA MJINI ATOA MCHANGO WA MIFUKO 200 YA SARUJI KWA SHULE YA SEKONDARI ITEZI


Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Mbeya Mjini Mhe. Dkt. Tulia Ackson, akikabidhi mifuko 200 ya saruji kwa Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari Itezi, Ndg. Betseba Nsemwa ikiwa ni mchango wake kwa Shule hiyo tukio lililofanyika leo Mkoani Mbeya, Februari 28, 2022, Kushoto ni Mstahiki Meya wa Jiji la Mbeya, Mhe. Dormohamed Rahmat na kulia ni Diwani wa kata ya Itezi, Mhe. Sambee Shitambala wengine ni Vijana kutoka Taasisi ya Tulia Trust


Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Mbeya Mjini Mhe. Dkt. Tulia Ackson, akisalimiana na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Itezi wakati alipowasili Shuleni hapo leo Mkoani Mbeya, Februari 28, 2022, kulia mbele ni Diwani wa kata ya Itezi, Mhe. Sambee Shitambala


Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Mbeya Mjini Mhe. Dkt. Tulia Ackson, akizungumza na wananchi na wanafunzi wa Shule ya Sekondari Itezi (hawapo kwenye picha) wakati alipoitembelea Shule hiyo leo Mkoani Mbeya, Februari 28, 2022, kushoto ni Mbunge wa Mchinga, Mhe. Salma Kikwete na Mstahiki Meya wa Jiji la Mbeya, Mhe. Dormohamed Rahmat


Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Itezi wakimsikiliza Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Mbeya Mjini Mhe. Dkt. Tulia Ackson, akizungumza wakati alipoitembelea Shule hiyo leo Mkoani Mbeya, Februari 28, 2022


Wananchi Mbalimbali wakimsikiliza Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mbunge wa Mbeya Mjini Mhe. Dkt. Tulia Ackson, akizungumza katika viwanja vya Shule ya Sekondari Itezi wakati alipoitembelea Shule hiyo leo Mkoani Mbeya, Februari 28, 2022



 

Sunday, February 27, 2022

SPIKA DKT. TULIA AZUNGUMZA NA WANANCHI WA JIJI LA MBEYA

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb), akisalimiana na viongozi mbalimbali wa kitaifa wakati alipowasili katika viwanja vya Ruanda Nzovwe leo Februari 27, 2022, kuzungumza na wananchi wa Jiji hilo 

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb), akizungumza na wananchi wa Jiji la Mbeya katika viwanja vya Ruanda Nzovwe leo Februari 27, 2022



Wananchi Mbalimbali wa Jiji la Mbeya wakimsikiliza Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb), akizungumza katika viwanja vya Ruanda Nzovwe leo Februari 27, 2022

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb), akizungumza na wananchi wa Jiji la Mbeya (hawapo kwenye picha) katika viwanja vya Ruanda Nzovwe leo Februari 27, 2022, Wengine ni Wabunge mbalimbali wa Mkoa wa Mbeya na Mikoa ya Jirani

Thursday, February 24, 2022

SPIKA DKT. TULIA AKUTANA A KUFANYA MAZUNGUMZO NA MAKAMU WA PILI WA RAIS ZANZIBAR

Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb), akizungumza na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla katika ofisi za Makamu wa Rais zilizopo Vuga Mjini Zanzibar, Februari 24, 2022


Spika wa Bunge, Mhe. Dkt.Tulia Ackson (Mb), katika picha ya pamoja na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla katika ofisi za Makamu wa Rais zilizopo Vuga Mjini Zanzibar, Februari 24, 2022



Spika wa Bunge, Mhe. Dkt.Tulia Ackson (Mb), akiagana na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla katika ofisi za Makamu wa Rais zilizopo Vuga Mjini Zanzibar, Februari 24, 2022

SPIKA DKT. TULIA ASHIRIKI SEMINA YA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAJUMBE WA KAMATI YA UONGOZI, MAKAMU WENYEVITI WA KAMATI NA TUME YA UTUMISHI WA BUNGE


Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb), akitolea ufafanuzi hoja mbalimbali za Wajumbe wa kamati ya uongozi, Makamu Wenyeviti wa kamati na Tume ya Utumishi wa Bunge katika semina ya mafunzo ya kuwajengea uwezo viongozi hao wa Wabunge yanayoendelea katika ofisi Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar, Februari 24, 2022, kulia ni Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mussa Zungu (Mb)



Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mussa Zungu (Mb), akiongoza semina ya mafunzo ya kuwajengea uwezo Wajumbe wa kamati ya uongozi, Makamu Wenyeviti wa kamati na Tume ya Utumishi wa Bunge yanayoendelea leo katika ofisi Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar, Februari 24, 2022, kushoto ni Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb)



Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi, Ndg. Kadari Singo akiwasilisha mada kuhusu misingi ya uongozi na utawala bora wakati wa semina ya mafunzo ya kuwajengea uwezo Wajumbe wa kamati ya uongozi, Makamu Wenyeviti wa kamati na Tume ya Utumishi wa Bunge yanayoendelea katika ofisi Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar, Februari 24, 2022



Baadhi ya Wajumbe wa kamati ya uongozi, Makamu Wenyeviti wa kamati na Tume ya Utumishi wa Bunge wakiwa katika semina ya mafunzo ya kuwajengea uwezo viongozi hao wa Bunge yanayoendelea katika ofisi Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar, Februari 24, 2022, kuanzia kushoto ni Wabunge wa Viti Maalum, Mhe. Halima Mdee, Mhe. Alice Kaijage na Mhe. Fatma Toufiq 



Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Bajeti, Mhe. Daniel Sillo (Mb), akichangia mada wakati wa majadiliano katika semina ya mafunzo ya kuwajengea uwezo Wajumbe wa kamati ya uongozi, Makamu Wenyeviti wa kamati na Tume ya Utumishi wa Bunge yanayoendelea katika ofisi Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar, Februari 24, 2022, kulia ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Dkt. Eliazer Feleshi, Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria na Mbunge wa Madaba, Mhe. Joseph Mhagama (kushoto)


 

Wednesday, February 23, 2022

NAIBU SPIKA MUSSA ZUNGU AONGOZA SEMINA YA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAJUMBE WA KAMATI YA UONGOZI, MAKAMU WENYEVITI WA KAMATI NA TUME YA UTUMISHI WA BUNGE


Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mussa Zungu (Mb), akiongoza semina ya mafunzo ya kuwajengea uwezo Wajumbe wa kamati ya uongozi, Makamu Wenyeviti wa kamati na Tume ya Utumishi wa Bunge yanayoendelea leo katika ofisi ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar, Februari 23, 2022, semina hiyo imewasilishwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mhe. Jumanne Sigini yenye mada kuhusu dhana ya mgawanyo wa madaraka na namna ya kudhibiti muingiliano wa madaraka ya mihimili ya dola

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mhe. Jumanne Sigini (Mb), akiwasilisha mada kuhusu dhana ya mgawanyo wa madaraka na namna ya kudhibiti muingiliano wa madaraka ya mihimili ya dola mbele ya Wajumbe wa kamati ya uongozi, Makamu Wenyeviti wa kamati na Tume ya Utumishi wa Bunge wakati wa semina ya mafunzo ya kuwajengea uwezo yanayoendelea leo katika ofisi ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar, Februari 23, 2022

Mwenyekiti wa kamati ya katiba na Sheria na Mbunge wa Madaba, Mhe. Joseph Mhagama (Mb), akichangia jambo wakati wa semina ya mafunzo ya kuwajengea uwezo Wajumbe wa kamati ya uongozi, Makamu Wenyeviti wa kamati na Tume ya Utumishi wa Bunge yanayoendelea leo katika ofisi ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar, Februari 23, 2022, semina hiyo imewasilishwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mhe. Jumanne Sigini yenye mada kuhusu dhana ya mgawanyo wa madaraka na namna ya kudhibiti muingiliano wa madaraka ya mihimili ya dola



Makamu Mwenyekiti wa kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge na Mbunge wa Jimbo la Tabora Kaskazini, Mhe. Almas Maige akichangia jambo wakati wa semina ya mafunzo ya kuwajengea uwezo Wajumbe wa kamati ya uongozi, Makamu Wenyeviti wa kamati na Tume ya Utumishi wa Bunge yanayoendelea leo katika ofisi ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar, Februari 23, 2022, semina hiyo imewasilishwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mhe. Jumanne Sigini yenye mada kuhusu dhana ya mgawanyo wa madaraka na namna ya kudhibiti muingiliano wa madaraka ya mihimili ya dola


 

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Dkt. Eliazer Feleshi akitoa ufafanuzi wakati wa semina ya mafunzo ya kuwajengea uwezo Wajumbe wa kamati ya uongozi, Makamu Wenyeviti wa kamati na Tume ya Utumishi wa Bunge yanayoendelea leo katika ofisi ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar, Februari 23, 2022, semina hiyo imewasilishwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mhe. Jumanne Sigini yenye mada kuhusu dhana ya mgawanyo wa madaraka na namna ya kudhibiti muingiliano wa madaraka ya mihimili ya dola

Tuesday, February 22, 2022

SPIKA DKT. TULIA ASHIRIKI MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO WAJUMBE WA KAMATI YA UONGOZI, MAKAMU WENYEVITI WA KAMATI NA TUME YA UTUMISHI WA BUNGE



Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson Mb, (katikati) akijibu hoja mbalimbali za Wajumbe wa kamati ya uongozi, Makamu Wenyeviti wa kamati na Tume ya Utumishi wa Bunge katika semina ya mafunzo ya kuwajengea uwezo viongozi hao wa Wabunge yanayoendelea katika ofisi Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar, Februari 22, 2022, kushoto ni Spika Mstaafu, Mhe. Pius Msekwa na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mussa Zungu (Mb)


Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mussa Zungu (Mb), akiongoza semina ya mafunzo ya kuwajengea uwezo Wajumbe wa kamati ya uongozi, Makamu Wenyeviti wa kamati na Tume ya Utumishi wa Bunge yanayoendelea leo katika ofisi Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar, Februari 22, 2022



Spika Mstaafu, Mhe. Pius Msekwa akiwasilisha mada kuhusu uzoefu, Changamoto na mbinu za uendeshaji bora wa vikao vya Bunge katika Bunge la Vyama vingi vya siasa katika semina ya mafunzo ya kuwajengea uwezo Wajumbe wa kamati ya uongozi, Makamu Wenyeviti wa kamati na Tume ya Utumishi wa Bunge yanayoendelea leo katika ofisi Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar, Februari 22, 2022, katika ni Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb) na Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Mussa Zungu (Mb)


Spika Mstaafu, Mhe. Anne Makinda akidadisi mada kuhusu uzoefu, Changamoto na mbinu za uendeshaji bora wa vikao vya Bunge katika Bunge la Vyama vingi vya siasa iliyowasilishwa na Spika Mstaafu, Mhe. Pius Msekwa katika semina ya mafunzo ya kuwajengea uwezo Wajumbe wa kamati ya uongozi, Makamu Wenyeviti wa kamati na Tume ya Utumishi wa Bunge yanayoendelea leo katika ofisi Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar, Februari 22, 2022


Spika Mstaafu wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mhe. Pandu Kificho akidadisi mada kuhusu uzoefu, Changamoto na mbinu za uendeshaji bora wa vikao vya Bunge katika Bunge la Vyama vingi vya siasa iliyowasilishwa na Spika Mstaafu, Mhe. Pius Msekwa katika semina ya mafunzo ya kuwajengea uwezo Wajumbe wa kamati ya uongozi, Makamu Wenyeviti wa kamati na Tume ya Utumishi wa Bunge yanayoendelea leo katika ofisi Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar, Februari 22, 2022


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama akiwasilisha mada kuhusu uzoefu na changamoto za uratibu wa Shughuli za Bunge na Shughuli za Serikali katika semina ya mafunzo ya kuwajengea uwezo Wajumbe wa kamati ya uongozi, Makamu Wenyeviti wa kamati na Tume ya Utumishi wa Bunge yanayoendelea leo katika ofisi Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar, Februari 22, 2022



Mwenyekiti wa Bunge, Mhe. David Kihenzile akichangia jambo wakati wa semina ya mafunzo ya kuwajengea uwezo Wajumbe wa kamati ya uongozi, Makamu Wenyeviti wa kamati na Tume ya Utumishi wa Bunge yanayoendelea leo katika ofisi Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar, Februari 22, 2022



Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Dkt. Eliazer Feleshi (kulia) pamoja na Waziri wa Nchi, ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu Balozi Mhe. Dkt. Pindi Chana wakishiriki katika semina ya mafunzo ya kuwajengea uwezo Wajumbe wa kamati ya uongozi, Makamu Wenyeviti wa kamati na Tume ya Utumishi wa Bunge yanayoendelea leo katika ofisi Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar, Februari 22, 2022

 

Monday, February 21, 2022

SPIKA DKT. TULIA AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MAKAMU WA KWANZA WA RAIS MIGOMBANI ZANZIBAR



Spika wa Bunge, Mhe. Dkt.Tulia Ackson akizungumza na Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Othman Masoud Othman katika ofisi za Makamu wa Rais Migombani Zanzibar, Februari 21, 2022



Spika wa Bunge, Mhe. Dkt.Tulia Ackson katika picha ya pamoja na Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Othman Masoud Othman katika ofisi za Makamu wa Rais Migombani Zanzibar, Februari 21, 2022



Spika wa Bunge, Mhe. Dkt.Tulia Ackson akiteta jambo na Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Othman Masoud Othaman katika ofisi za Makamu wa Rais Migombani Zanzibar, Februari 21, 2022


Spika wa Bunge, Mhe. Dkt.Tulia Ackson akiagana na Makamu wa kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Othman Masoud Othaman katika ofisi za Makamu wa Rais Migombani Zanzibar, Februari 21, 2022

SPIKA DKT. TULIA AFUNGUA MAFUNZO YA SIKU 5 KWA KAMATI YA UONGOZI, MAKAMU WENYEVITI WA KAMATI NA TUME YA UTUMISHI WA BUNGE


Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb) akifungua semina ya mafunzo ya siku 5 ya kuwajengea uwezo Wajumbe wa kamati ya uongozi, Makamu Wenyeviti wa kamati na Tume ya Utumishi wa Bunge (hawapo kwenye picha) katika ofisi Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar, Februari 21, 2022 


Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb) akifungua semina ya mafunzo ya siku 5 ya kuwajengea uwezo Wajumbe wa kamati ya uongozi, Makamu Wenyeviti wa kamati na Tume ya Utumishi wa Bunge katika ofisi Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar, Februari 21, 2022 



Katibu wa Bunge, Ndg. Nenelwa Mwihambi akizungumza kabla ya Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb), kufungua semina ya mafunzo ya siku 5 ya ya kuwajengea uwezo Wajumbe wa kamati ya uongozi, Makamu Wenyeviti wa kamati na Tume ya Utumishi wa Bunge katika ofisi ndogo za Bunge Tunguu, Zanzibar, Februari 21, 2022, kuanzia kushoto ni Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mhe. Zuberi Ali Maulid, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mussa Zungu




Baadhi ya Wajumbe wa kamati ya uongozi wakishiriki mafunzo ya siku 5 ya kuwajengea uwezo Wajumbe wa kamati ya uongozi, Makamu Wenyeviti wa kamati na Tume ya Utumishi wa Bunge katika ofisi Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar, Februari 21, 2022, Mafunzo hayo yamefunguliwa leo na Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson(Mb)



Spika wa Bunge, Mhe.Dkt. Tulia Ackson Mb, (katikati waliokaa) katika picha ya pamoja na kamati ya uongozi baada ya kufungua mafunzo ya siku 5 ya kuwajengea uwezo Wajumbe wa kamati ya uongozi, Makamu Wenyeviti wa kamati na Tume ya Utumishi wa Bunge katika ofisi Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar, Februari 21, 2022, kuanzia kushoto waliokaa ni Spika Mstaafu, Mhe. Anne Makinda, Spika Mstaafu, Mhe. Pius Msekwa, Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mhe. Zuberi Ali Maulid, Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mussa Zungu, Spika Mstaafu wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mhe. Pandu kificho na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Dkt. Eliazer Feleshi



 

Saturday, February 19, 2022

SPIKA DKT. TULIA ASHIRIKI ZOEZI LA KUAGA MWILI WA DKT. MWELECELE KARIMJEE JIJINI DAR ES SALAAM


Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb), akiaga mwili wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Udhibiti wa Magonjwa ya Kitropiki yasiyopewa kipaumbele wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Dkt. Mwelecele Ntuli Malecela katika viwanja vya karimjee Jijini Dar es Salaam, Februari 19, 2022


Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb), akiteta jambo na Spika Mstaafu, Mhe. Anne Makinda wakati wa zoezi la kuaga mwili wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Udhibiti wa Magonjwa ya Kitropiki yasiyopewa kipaumbele wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Dkt. Mwelecele Ntuli Malecela katika viwanja vya karimjee Jijini Dar es Salaam, Februari 19, 2022

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb), wakati alipowasili kuaga mwili wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Udhibiti wa Magonjwa ya Kitropiki yasiyopewa kipaumbele wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Dkt. Mwelecele Ntuli Malecela katika viwanja vya karimjee Jijini Dar es Salaam, Februari 19, 2022

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi (wapili kulia), Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa (kulia), Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson Mb, (wapili kushoto) pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Amos Makalla wakishiriki zoezi la kuaga mwili wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Udhibiti wa Magonjwa ya Kitropiki yasiyopewa kipaumbele wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Dkt. Mwelecele Ntuli Malecela katika viwanja vya karimjee Jijini Dar es Salaam, Februari 19, 2022


Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb), akitoa salamu za rambirambi wakati wa kuaga mwili wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Udhibiti wa Magonjwa ya Kitropiki yasiyopewa kipaumbele wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Dkt. Mwelecele Ntuli Malecela katika viwanja vya karimjee Jijini Dar es Salaam, Februari 19, 2022


 

Friday, February 18, 2022

SPIKA DKT. TULIA AZINDUA KADI MPYA ZA UANACHAMA ZA KIELEKTRONIKI ZA KLABU YA YANGA



Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb), akizungumza na viongozi wa Klabu ya Yanga na Wabunge wapenzi wa Yanga katika hafla fupi ya uzinduzi wa kadi mpya ya uanachama ya kielektroniki ya klabu ya Yanga iliyofanyika leo katika hoteli ya Nashera Jijini Dodoma, Februari 18, 2022, Kuanzia kushoto ni Mkurugenzi wa uwekezaji wa Klabu ya Yanga, Injinia Hersi Said, Meneja wa timu ya Bunge Sports Club, Mhe. Seif Gulamali, Afisa Mtendaji Mkuu wa Klabu ya Yanga, Ndg. Senzo Mazingiza na Waziri ofisi ya Rais Kazi Maalum Mhe. Cpt. George Mkuchika



Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb), akizungumza na viongozi wa Klabu ya Yanga na Wabunge wapenzi wa Yanga katika hafla fupi ya uzinduzi wa kadi mpya ya uanachama ya kielektroniki ya klabu ya Yanga iliyofanyika leo katika hoteli ya Nashera Jijini Dodoma, Februari 18, 2022, Kuanzia kushoto ni Mkurugenzi wa uwekezaji wa Klabu ya Yanga, Injinia Hersi Said, Meneja wa timu ya Bunge Sports Club, Mhe. Seif Gulamali, Afisa Mtendaji Mkuu wa Klabu ya Yanga, Ndg. Senzo Mazingiza na Waziri ofisi ya Rais Kazi Maalum Mhe. Cpt. George Mkuchika


Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb), akimkabidhi Waziri ofisi ya Rais Kazi Maalum Mhe. Cpt. George Mkuchika kadi namba moja ya uanachama ya kielektroniki kwa klabu ya Yanga katika hafla fupi ya uzinduzi iliyofanyika leo katika hoteli ya Nashera Jijini Dodoma, Februari 18, 2022


Waziri ofisi ya Rais Kazi Maalum Mhe. Cpt. George Mkuchika akimkabidhi jezi ya Klabu ya Yanga Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb), katika hafla fupi ya uzinduzi wa kadi mpya ya uanachama ya kielektroniki ya klabu ya Yanga iliyofanyika leo katika hoteli ya Nashera Jijini Dodoma, Februari 18, 2022



Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb), katika picha ya pamoja na viongozi wa Klabu ya Yanga na Wabunge wapenzi wa Yanga katika hafla fupi ya uzinduzi wa kadi mpya ya uanachama ya kielektroniki ya klabu ya Yanga iliyofanyika leo katika hoteli ya Nashera Jijini Dodoma, Februari 18, 2022, Watatu kushoto mbele ni Waziri ofisi ya Rais Kazi Maalum Mhe. Cpt. George Mkuchika, Mwenyekiti wa timu ya Bunge Sports Club, Mhe. Tarimba Abbas (kulia mbele), na Meneja wa timu ya Bunge Sports Club, Mhe. Seif Gulamali (wapili kulia) 



SPIKA DKT. TULIA AFANYA MAZUNGUMZO NA MKURUGENZI MKUU WA HOSPITALI YA BENJAMIN MKAPA, MKURUGENZI ASAS DIARIES NA UONGOZI WA BENKI YA WATU WA ZANZIBAR TAWI LA DODOMA

Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb), akizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Benjamin Mkapa, Dkt. Alphonce Chandika alipomtembelea leo ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma, Februari 18, 2022


Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson Mb, (watatu kulia) katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Benjamin Mkapa, Dkt. Alphonce Chandika (watatu kushoto) alieambatana na watendaji kutoka hospitali hiyo walipomtembelea leo ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma, Februari 18, 2022


Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (Mb), akizungumza na Mkurugenzi wa uzalishaji wa kampuni ya maziwa ya ASAS, Ndg. Ahmed Salim Abri alipomtembelea leo ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma, Februari 18, 2022


Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson Mb, (kushoto) akizungumza na Meneja wa Benki ya Watu wa Zanzibar tawi la Dodoma, Ndg. Mohamed Masoud (wakwanza kushoto) alieambatana na Maafisa kutoka Benki hiyo walipomtembelea leo ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma, Februari 18, 2022



 

Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson Mb, (kushoto) akipokea zawadi kutoka kwa Meneja wa Benki ya Watu wa Zanzibar Tawi la Dodoma, Ndg. Mohamed Masoud alipomtembelea leo ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma, Februari 18, 2022