WELCOME TO TANZANIA NATIONAL ASSEMBLY OFFICIAL BLOG: CONTACT US: P.O.BOX 941 DODOMA, TANZANIA, WEBSITE: parliament.go.tz , FIND US ON FACEBOOK >>> www.facebook.com/bungetz1, FOLLOW US ON TWITTER >>> @bunge_tz.>>>KARIBUNI

Wednesday, June 30, 2021

BUNGE LAAHIRISHWA HADI AGOSTI 31, 2021


 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisoma hotuba ya kuahirisha Mkutano wa 3 wa Bunge la 12 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Bungeni jijini Dodoma, Juni 30, 2021.

                                                    -----

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema ili kuhakikisha bajeti ya 2021/2022 inatoa matokeo yaliyokusudiwa, Serikali itaimarisha matumizi ya mifumo ya kielektroniki kwa ajili ya kuongeza uwazi na uwajibikaji na hivyo kudhibiti matumizi ya fedha za umma kwa kuepuka malipo hewa na manunuzi ya umma ya bidhaa na huduma zisizokidhi viwango vya ubora.

Ameyasema hayo leo (Jumatano, Juni 30, 2021) wakati akiahirisha mkutano wa tatu wa Bunge la 12, Bungeni jijini Dodoma. Bunge limeahirishwa hadi Agosti 31 mwaka huu.

Amesema Serikali itahakikisha uwepo wa thamani halisi ya matumizi ya fedha za umma katika utekelezaji wa miradi ikiwa ni pamoja na kuchukua hatua stahiki tena kwa wakati pale inapobaini ukiukwaji wa sheria, taratibu na kanuni za matumizi ya fedha za umma.

“Utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa mwaka 2021/2022 unakwenda sambamba na Mikakati ya Serikali katika kuimarisha udhibiti wa matumizi ya fedha za umma, utendaji na uwajibikaji kwa viongozi na watendaji wote wa sekta ya umma. Hatua hizo, zinalenga kuhakikisha bajeti hii inatoa matokeo yaliyokusudiwa.”

Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwasisitiza watendaji wa Serikali hususan wa Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) wajipange vema na wahakikishe suala la posho za madaraka kwa watendaji wa kata na vijiji kupitia mpango wa halmashauri linasimamiwa na kutekelezwa ipasavyo.

Kadhalika, Waziri Mkuu amewataka watendaji wa Mamlaka za Serikali za Mitaa wahakikishe wanatenga maeneo maalumu kwa ajili ya vijana na wafanyabiashara wadogo sambamba na kuwapatia elimu pamoja na kuwashirikisha katika kubaini maeneo yanayoendana na biashara zao. Amewaagiza watendaji hao wasikilize na kushughulikia kero za wananchi kwa wakati ikiwa ni pamoja na kutenga siku maalum kwa ajili hiyo.

Wakati huo huo, Waziri Mkuu  amesema utaratibu wa utoaji wa vibali vya ukaazi kwa kutumia mfumo wa kielektroniki umesaidia kupunguza hatua za kuchakata maombi kutoka siku 33 za hadi saba.

Amesema kuwa kwa sasa waombaji hawalazimiki kwenda katika Ofisi za Kazi kwa sababu taarifa zote zinapatikana kwenye mfumo na watajaza fomu moja tu ambayo huwa na taarifa zote za kazi na ukaazi tofauti na awali ambapo wawekezaji walilazimika kujaza fomu mbili.

Ameyasema hayo leo (Jumatano, Juni 30, 2021) wakati akiahirisha mkutano wa tatu wa Bunge la 12, Bungeni jijini Dodoma. Bunge limeahirishwa hadi Agosti 31 mwaka huu.

Amesema miongoni mwa manufaa yaliyopatikana kupitia matumizi ya mfumo huo ni kupungua kwa siku za kushughulikia maombi ya vibali vya kazi kutoka siku 14 hadi siku tatu. “Hali hii, pamoja na mambo mengine, imesaidia kupunguza malalamiko ya kuchelewa kupata majibu ya maombi ya vibali vya kazi.”

Hata hivyo, Waziri Mkuu amesema Serikali inaendelea kupokea maoni kutoka kwa watumiaji wa mfumo kwa ajili ya maboresho na tayari imeshakutana na kupokea maoni ya wadau wa ndani na nje kikiwemo Chama cha Wafanyakazi, Chama cha Waajiri (ATE), Shirikisho la Wenye Viwanda (CTI), Taasisi ya Sekta Binafsi na kuyajumuisha maoni hayo kwenye maboresho.

Amesema Serikali inakamilisha maboresho ya Sheria ya Kuratibu Ajira za Wageni (Sura 436) kwa kuainisha maeneo yaliyokuwa na changamoto za kiutendaji na kuathiri jitihada za kuimarisha mazingira ya uwekezaji nchini. Mfumo huo unatarajiwa kuzinduliwa rasmi Agosti mwaka huu.

“Sambamba na marekebisho hayo ya sheria, tangu tarehe 23 Aprili, 2021 tumeanza kutumia mfumo wa kielektroniki wa kushughulikia maombi ya vibali vya kazi kwa raia wa kigeni na katika hatua za majaribio tayari maombi zaidi ya 500 yameshughulikiwa kupitia mfumo huo.”


WABUNGE WANAWAKE NA WATUMISHI OFISI YA BUNGE WANAWAKE WAMPONGEZA MWANAMKE WAKWANZA ALIYETEULIWA KUWA KATIBU WA BUNGE

Wajumbe wa Chama cha Wabunge Wanawake (TWPG) wakimpatia zawadi  Bi. Nenelwa Mwihambi (wa pili kushoto) ya pongezi kwa kuteuliwa na Mheshimiwa Rais kuwa Katibu wa Bunge katika tukio lililofanyika ukumbi wa Pius Msweka Jijini Dodoma.

Mwenyekiti wa Chama cha Wabunge Wanawake (TWPG), Mhe. Shally Raymond (wa pili kushoto) akizungumza wakati wa tukio la kumpongeza Bi. Nenelwa Mwihambi  kwa kuteuliwa na Mheshimiwa Rais kuwa Katibu wa Bunge katika ukumbi wa Pius Msweka Jijini Dodoma.

Katibu wa Bunge, Bi. Nenelwa Mwihambi akizungumza wakati wa tukio la kumpongeza kwa kuteuliwa na Mheshimiwa Rais kuwa Katibu wa Bunge katika ukumbi wa Pius Msweka Jijini Dodoma.

Wanawake Watumishi wa Ofisi ya Bunge wakimpatia zawadi ya pongezi Bi. Nenelwa Mwihambi (wa tatu kushoto) kwa kuteuliwa na Mheshimiwa Rais kuwa Katibu wa Bunge katika tukio lililofanyika ukumbi wa Pius Msweka Jijini Dodoma.

 

 

BUNGE LA 12 MKUTANO WA TATU KIKAO CHA 62, TAREHE 30.06.2021


 

Thursday, June 24, 2021

WABUNGE WAPEWA SEMINA KUHUSU MICHEZO YA KUBAHATISHA


Naibu Spika wa Bunge,Mheshimiwa Dkt. Tulia Ackson akizungumza akipokuwa akifungua semina ya wabunge kuhusu makampuni yanayojihusisha na michezo ya kubahatisha jinsi yanavyofanya kazi zao hapa nchini na mchango wao katika uchumi wa nchi, iliyofanyika jijini Dodoma jana

Mwenyekiti wa Chama cha Waendesha Michezo ya Kubahatisha nchini, Jimmy Brian akitoa mada katika semina ya wabunge kuhusu michezo ya kubahatisha inavyofanyika hapa nchini na mchango wao katika kukuza uchumi wa nchi, iliyofanyika jijini Dodoma jana.


BUNGE LA 12 MKUTANO WA TATU KIKAO CHA 58, TAREHE 24.06.2021


 

Tuesday, June 22, 2021

BUNGE LAPITISHA BAJETI KUU YA SERIKALI


 

BUNGE limepitisha Bajeti Kuu ya Serikali ya shilingi trilioni 36.68 kwa mwaka wa fedha 2021/2022 ambapo Wabunge 361 sawa na asilimia 94 wamepiga kura ya ndio.

Akitangaza matokeo ya upigaji wa kura mara baada ya mjadala wa Bajeti ya Serikali uliofanyika kwa takribani wiki moja Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai amesema kuwa Wabunge waliopiga kura ni 385 ambapo waliopiga kura ya Ndio ni 361 sawa na asilimia 94, waliopiga kura isiyo ya maamuzi (hawajakataa wala kukubali) ni 23 sawa na asilimia 6 na Wabunge watano (5) hawakuwepo wakati wa zoezi hilo la upigaji kura. 

Aidha, mara baada ya upigaji huo wa kura Bunge lilipitisha Muswada wa Sheria ya kuidhinisha Matumizi ya Serikali wa mwaka 2021 (The Appropriation Bill, 2021) wenye dhumuni la kuidhinisha Matumizi ya jumla ya Shilingi 36,681,897,765,000.

Mara baada ya kupitisha Bajeti zote za Wizara pamoja na Bajeti kuu ya Serikali, Mkutano wa Tatu wa Bunge unatarajia kuendelea na ukamilishaji wa shughuli zilizobaki za Kiserikali na Kamati kabla ya kuahirishwa Juni 30, 2021.

BUNGE LA 12 MKUTANO WA TATU KIKAO CHA 56, TAREHE 22.06.2021


 

Monday, June 21, 2021

WAPEWA MAFUNZO JUU YA HALI HALISI YA MALEZI, MAKUZI NA MAENDELEO YA AWALI YA MTOTO NCHINI

Mwakilishi wa Shirika la Elizabeth Glacies Foundation Ndg. Josephine Ferla akiwasilisha mada kwenye Semina ya Wabunge juu ya Hali ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Morena Jijini Dodoma. 

Naibu Waziri wa Afya anayeshughulikia Maendeleo ya Jamii,  Mhe. Mwanaidi Ali Khamis akifafanua jambo kwenye Semina ya Wabunge juu ya Hali ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto hii leo Jijini Dodoma. 

Mbunge wa Momba Mhe.  Condester Sichalwe akichangia jambo kwenye Semina ya Wabunge juu ya Hali ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto hii leo Jijini Dodoma. 


BUNGE LA 12 MKUTANO WA TATU KIKAO CHA 55, TAREHE 21.06.2021


 

Saturday, June 19, 2021

SPIKA NDUGAI AZINDUA RIPOTI YA BAJETI ZA LISHE KATIKA NCHI ZA MASHARIKI NA KUSINI MWA AFRIKA

Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai akizindua ripoti ya uchambuzi wa bajeti za lishe kwa nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika katika ukumbi wa Msekwa, Bungeni, Jijini Dodoma. Kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Wabunge Vinara wa Lishe, salama wa chakula na haki za Watoto Bungeni Mhe. Dustan Kitandura, Mtaalam mwandamizi wa lishe kutoka Mradi wa ASPIRES, Tumaini Charles na kulia kwake ni Mkurungenzi Mtendaji PANITA, Tumaini Mikindo. 



Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai akisisitiza jambo kwa Wabunge Vinara wa lishe, Usalama wa chakula na haki za Watoto Bungeni alipozungumza nao katika mkutano kuhusu masuala ya lishe uliofanyika katika ukumbi wa Msekwa, Bungeni, Jijini Dodoma mkutano ambao ulizindua ripoti ya uchambuzi wa bajeti za lishe kwa nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika


Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai akionyesha ripoti ya uchambuzi wa bajeti za lishe kwa nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika aliyoizindua katika ukumbi wa Msekwa, Bungeni, Jijini Dodoma. Kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Wabunge Vinara wa lishe, usalama wa chakula na haki za Watoto Bungeni Mhe. Dustan Kitandura, Mtaalam mwandamizi wa lishe kutoka Mradi wa ASPIRES, Tumaini Charles na kulia kwake ni Mkurungenzi Mtendaji PANITA, Tumaini Mikindo. 

Kikundi cha Wabunge Vinara wa Lishe, Usalama wa Chakula na Haki za Watoto Bungeni wakimsikiliza Spika wa Bunge Mhe Job Ndugai alipozungumza nao katika mkutano kuhusu masuala ya lishe uliofanyika katika ukumbi wa Msekwa, Bungeni, Jijini Dodoma mkutano ambao ulizindua ripoti ya uchambuzi wa bajeti za lishe kwa nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika iliyoandaliwa na Mradi wa lishe wa ASPIRES ulio chini ya Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Marekani (USAID).   


Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama, akizungumza na Wabunge Vinara wa Lishe, Usalama wa Chakula na Haki za Watoto Bungeni katika mkutano wa masuala ya lishe uliofanyika katika ukumbi wa Msekwa, Bungeni, Jijini Dodoma.

HALMASHAURI ZASHAURIWA KUONGEZA FEDHA KATIKA BAJETI ZA LISHE 

Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai ameshauri Halmashauri nchi kuongeza fedha zinazotengwa kwa ajili ya masuala ya lishe kwa watoto wa umri wa chini ya miaka mitano katika Bajeti zijazo kwa sababu fedha zinazotengwa sasa bado hazikidhi mahitaji yote.

Mhe. Ndugai aliyasema hayo jana wakati akizindua ripoti ya uchambuzi wa bajeti za lishe kwa nchi za mashariki na kusini mwa Afrika nchini katika mkutano wa wabunge vinara wa lishe, usalama wa chakula na haki za watoto Bungeni ulioandaliwa na taasisi zinayoshughulika na lishe za Panita na  Mradi wa lishe wa Aspires uliopo chini ya Shirika la Kimataifa la Maendeleo la Marekani (USAID).

Mheshimiwa Spika Ndugai alisema ingawa bado kiwango hicho hakikidhi mahitaji yote ya watoto lakini ni hatua nzuni na kushauri kuendelea kuongeza kiwango katika bajeti zijazo.

“Ni wito wangu kwa TAMISEMI (Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za mitaa) kuhakikisha kuwa fedha hizo zinazotengwa katika bajeti za halmashauri zinatolewa kikamilifu na kwa wakati,”alisema.

Kwa upande wake Mtaalam Mwandamizi wa Lishe katika Mradi wa Asprires, Tumaini Charles alisema kuna kasi ya ongezeko la watu wenye uzito na kiriba tumbo na kuongeza kuwa  tatizo hilo lipo kwa kiasi kikubwa kwa watu wenye elimu ya  sekondari na kuendelea na familia zenye maisha mazuri.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa TANITA, Tumaini Mkindo alishauri Serikali kuangalia jinsi ya kuweka pamoja mipango ya afua za udumavu na uzito mkubwa kwa sababu mtoto aliyekabiliwa udumavu kuwa katika uwezekano wa kupata magonjwa mengine kama ugonjwa wa moyo.

Mwenyekiti wa kikundi hicho Mhe.  Danstun Kitandula alisema ni vizuri fedha zinazotengwa kwa ajili ya afua za lishe kuwekewa uzio ili zisitumike katika shughuli nyingine.

“Fedha zinazotengwa kwa ajili ya lishe huwa hazikaguliwi na CAG (Mthibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali) tunashauri aweke jicho lake kwenye eneo hilo kwa sababu athari yake ni kubwa,” alisema.

Mwisho

Saturday, June 12, 2021

SPIKA NDUGAI ASHIRIKI SEMINA KUHUSU UFANISI WA RANCHI ZA TAIFA

Mjumbe wa Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji Mhe. Dkt. Bashiru Ally akichangia jambo kwenye Semina kuhusu Ufanisi wa Ranchi za Taifa iliyotolewa kwa Wajumbe wa Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji kwenye Ukumbi wa Msekwa Bungeni Jijini Dodoma. 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Elisante Ole Gabriel akifafanua jambo kwenye Semina kuhusu Ufanisi wa Ranchi za Taifa iliyotolewa kwa Wajumbe wa Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji kwenye Ukumbi wa Msekwa Bungeni Jijini Dodoma.


Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe.
Abdallah Ulega  akifafanua jambo kwenye Semina kuhusu Ufanisi wa Ranchi za Taifa iliyotolewa kwa Wajumbe wa Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji kwenye Ukumbi wa Msekwa Bungeni Jijini Dodoma. 


Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji  Mhe. Dkt. Christine Ishengoma akichania jambo kwenye Semina kuhusu Ufanisi wa Ranchi za Taifa iliyotolewa kwa Wajumbe wa Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji kwenye Ukumbi wa Msekwa Bungeni Jijini Dodoma. 



Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai akifafanua jambo kwenye Semina kuhusu Ufanisi wa Ranchi za Taifa. Katika Semina hiyo Mhe Spika alitoa uzoefu wake kama Mbunge wa Kongwa kuhusu ufanisi wa Ranchi ya Kongwa kabla na baada ya uhuru. 



Sunday, June 6, 2021

WABUNGE WANAWAKE WAPEWA MAFUNZO NA LHRC JUU YA NAFASI YA MWANAMKE KAMA KIONGOZI

Sehemu ya Wabunge wakifuatilia kwa karibu kwenye Mafunzo ya Wabunge Wanawake juu ya nafasi ya mwanamke kama Kiongozi iliyofanyika hii leo kwenye ukumbi wa Msekwa Bungeni Jijini Dodoma hii leo. 
Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Dkt. Anna Mghwira akielezea jambo alipokuwa akitoa Mada juu ya nafasi ya Kiongozi Mwanamke katika ngazi mbalimbali kwa Wabunge Wanawake iliyofanyika kwenye ukumbi wa Msekwa Bungeni Jijini Dodoma hii leo. 


Naibu Spika wa Bunge Mhe. Dkt. Tulia Ackson akifafanua jambo alipokuwa akitoa mada juu ya Maadili na Kanuni za Bunge kwa Wabunge Wanawake iliyofanyika kwenye ukumbi wa Msekwa Bungeni Jijini Dodoma hii leo. 

Naibu Spika wa Bunge Mhe. Dkt. Tulia Ackson akifafanua jambo alipokuwa akitoa mada juu ya Maadili na Kanuni za Bunge kwa Wabunge Wanawake iliyofanyika kwenye ukumbi wa Msekwa Bungeni Jijini Dodoma hii leo.