WELCOME TO TANZANIA NATIONAL ASSEMBLY OFFICIAL BLOG: CONTACT US: P.O.BOX 941 DODOMA, TANZANIA, WEBSITE: parliament.go.tz , FIND US ON FACEBOOK >>> www.facebook.com/bungetz1, FOLLOW US ON TWITTER >>> @bunge_tz.>>>KARIBUNI

Tuesday, October 3, 2023

TIMU ZA BUNGE ZAENDELEA KUFANYA VIZURI KATIKA MICHEZO YA SHIMIWI MKOANI IRINGA





Timu za Klabu ya michezo za Bunge zimeendelea kufanya vizuri katika michezo ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI) inayoendelea leo tarehe 3 Oktoba Mkoani Iringa.

Timu ya kamba wanawake imeigaragaza timu ya Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa pointi 2-0 huku timu ya kamba wanaume ikiiburuza timu ya Ujenzi kwa pointi 1-0 wakati wa mchezo uliofanyika katika viwanja vya Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Mkwawa.

Nayo timu ya netiboli imeibuka kidedea baada ya kuibugiza magoli 31 - 16 timu ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum wakati wa mchezo uliofanyika katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCU).

Kwa upande wa timu ya soka ya Bunge imeicharaza goli 2 -1 timu ya soka ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa wakati wa mchezo uliofanyika katika uwanja wa CCM Samora Mkoani hapa.

Michezo SHIMIWI inaendelea kutimua vumbi Katika viwanja mbalimbali na inategemewa kuhitimishwa tarehe 14 Oktoba, 2023, Mkoani Iringa.

No comments:

Post a Comment