WELCOME TO TANZANIA NATIONAL ASSEMBLY OFFICIAL BLOG: CONTACT US: P.O.BOX 941 DODOMA, TANZANIA, WEBSITE: parliament.go.tz , FIND US ON FACEBOOK >>> www.facebook.com/bungetz1, FOLLOW US ON TWITTER >>> @bunge_tz.>>>KARIBUNI

Thursday, January 4, 2024

SPIKA DKT. TULIA ASHIRIKI HAFLA YA UFUNGUZI WA KONGAMANO LA 27 LA MASPIKA NA WENYEVITI WA MABUNGE YA JUMUIYA YA MADOLA






Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson ameshiriki hafla ya ufunguzi wa Kongamano la 27 la Maspika na Wenyeviti wa Mabunge ya Jumuiya ya Madola uliofanyika leo tarehe 4 Januari, 2024, Kampala nchini Uganda.

Kongamano hilo limefunguliwa na Rais wa nchi hiyo Mhe. Jenerali Yoweri Kaguta Museveni.

Kongamano hilo pamoja na mambo mengine linatoa fursa kwa Maspika kubadilishana uzoefu wa  uendeshaji bora wa Mabunge. Katika Kongamano hilo linaloendelea hadi tarehe 6 Januari 2024, mada mbalimbali zitawasilishwa na kujadiliwa ikiwemo masuala ya mazingira na mabadiliko ya tabia nchi, masuala ya jinsia na ushirikishwaji wa vijana pamoja na ujengaji wa misimamo ya pamoja ya kibunge.


 

No comments:

Post a Comment