WELCOME TO TANZANIA NATIONAL ASSEMBLY OFFICIAL BLOG: CONTACT US: P.O.BOX 941 DODOMA, TANZANIA, WEBSITE: parliament.go.tz , FIND US ON FACEBOOK >>> www.facebook.com/bungetz1, FOLLOW US ON TWITTER >>> @bunge_tz.>>>KARIBUNI

Tuesday, August 29, 2017

WAJUMBE WA KAMATI YA BAJETI WATEMBELEA MRADI WA MABASI YA MWENDOKASI KUANGALIA MFUMO WA UKUSANYAJI NAULI



Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Bajeti, Mhe. Hawa Ghasia akielekezwa jinsi ya kutumia risiti ya Mwendokasi kwa ajili ya kuingia kituoni kusubiri basi.

Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Bajeti wakiwa ndani ya Basi la Mwendo Kasi wakielekea Hospitali ya Muhimbili Jijini Dar es Salaam, wajumbe hao walikuwa wakikagua mfumo wa kukusanya fedha za nauli kwa mabasi hayo uliotengenezwa na Kampuni ya Maxcom.

Saturday, August 26, 2017

KAMATI YA BUNGE YA BAJETI YATEMBELEA KIWANDA CHA SARUJI CHA DANGOTE NA BANDARI YA MTWARA

Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya  Bajeti wakikagua mradi wa ujenzi wa Gati jipya la Bandari ya Mtwara.




Kaimu Mkurugenzi Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Karim Mattaka  akitoa maelezo kwa Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Bajeti kuhusiana na Bandari ya Mtwara na mradi upanuzi wa Gati jipya unaoendelea hivi sasa wakati wajumbe hao walipotembelea Bandari hiyo.

Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Bajeti wakisikiliza maelezo kutoka kwa Injinia wa uzalishaji wa  Kiwanda cha Saruji cha Dangote kuhusu kiwanda hicho kinavyofanya kazi wakati wajumbe hao walipofanya ziara katika Kiwanda hicho kichopo Mkoa wa Mtwara


Mkurugenzi Mkazi wa Kiwanda cha Saruji cha Dangote, Hemendra Raithatha akitoa maelezo kuhusiana na Kiwanda hicho kwa Kamati ya Bunge ya Bajeti wakati Kamati hiyo ilipotembelea Kiwanda hicho kilichopo Mkoani Mtwara.
Wajumbe wa Kamati Bunge ya Bajeti wakikagua eneo la machimbo ya ‘lime stone’ ambayo Kiwanda cha Saruji Dangote kinachimba kwa ajili ya kutengenezea saruji