WELCOME TO TANZANIA NATIONAL ASSEMBLY OFFICIAL BLOG: CONTACT US: P.O.BOX 941 DODOMA, TANZANIA, WEBSITE: parliament.go.tz , FIND US ON FACEBOOK >>> www.facebook.com/bungetz1, FOLLOW US ON TWITTER >>> @bunge_tz.>>>KARIBUNI

Sunday, June 28, 2020

SPIKA AKABIDHI KOMPYUTA 20 SHULE ZA SEKONDARI WILAYA YA KONGWA

Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akizungumza hafla ya makabidhiano ya Kompyuta 20 alizozitoa kwa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa kwa ajili ya shule za sekondari za Wilaya hiyo, kushoto ni Mkurugenzi wa Elimu TAMISEMI, Ndugu Julius Nestory na kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kongwa aliyemaliza muda wake Ndugu White Zuberi.Hafla hiyo imefanyika katika Ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa.

Mkurugenzi wa Elimu TAMISEMI, Ndugu Julius Nestory akizungumza katika hafla ya makabidhiano ya Kompyuta 20 zilizotolewa na Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai kwa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa kwa ajili ya shule za sekondari za Wilaya hiyo, katikati ni Mheshimiwa Spika na kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kongwa aliyemaliza muda wake Ndugu White Zuberi.Hafla hiyo imefanyika katika Ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa.

Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akikabidhi kompyuta kwa baadhi ya wakuu wa shule za sekondari za Wilaya ya Kongwa katika hafla ambayo ilihudhuriwa pia na baadhi ya viongozi wakiwemo Mkurugenzi wa Elimu TAMISEMI, Ndugu Julius Nestory, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kongwa aliyemaliza muda wake Ndugu White Zuberi na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Dkt. Omary Nkulo

Friday, May 8, 2020

KAMATI YA KILIMO YAKUTANA NA WADAU WA KILIMO CHA MBOGA, MATUNDA, VIUNGO NA MAUA JIJINI DODOMA

Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji Mheshimiwa Mahmoud Mgimwa akifafanua jambo mbele ya Kamati hiyo ilipokutana na Wadau mbalimbali kujadili hali ya maendeleo katika kilimo cha Mbogamboga, Matunda, Viungo na Maua hapa nchini kilichofanyika Jijini Dodoma hii leo.

Waziri wa Kilimo Mheshimiwa Japhet Hasunga akifafanua jambo mbele ya Kamati ya kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji ilipokutana na Wadau mbalimbali kujadili hali ya maendeleo katika kilimo cha Mbogamboga, Matunda, Viungo na Maua hapa nchini kilichofanyika Jijini Dodoma hii leo. 

Wajumbe wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji wakifuatilia kwa makini mjadala wa Kamati hiyo ilipokutana na Wadau mbalimbali kujadili hali ya maendeleo katika kilimo cha Mbogamboga, Matunda, Viungo na Maua hapa nchini kilichofanyika Jijini Dodoma hii leo. 

Mjumbe wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji Mheshimiwa Dkt. Ritta Kabati akichangia jambo kwenye mjadala wa Kamati hiyo ilipokutana na Wadau mbalimbali kujadili hali ya maendeleo katika kilimo cha Mbogamboga, Matunda, Viungo na Maua hapa nchini kilichofanyika Jijini Dodoma hii leo. 

Thursday, April 30, 2020

WABUNGE WANAWAKE WAPATIWA MAFUNZO KUHUSU YA SHERIA ZA MIRATHI



Afisa wa Bunge Ndg. Seraphine Tamba akifafanua jambo alipokuwa akitoa mada kwenye Kikao cha kuwawezesha Wabunge Wanawake juu ya Uelewa wa Utata na Uwiano usio sawa wa Mgawanyo wa Mirathi kwa Wajane na Wagane (Sheria za Mirathi) kwenye Ukumbi wa Msekwa Bunge Jijini Dodoma hii leo.
Mwenyekiti wa Umoja wa Wabunge Wanawake (TWPG) Mheshimiwa Margret Sitta akifafanua jambo alipokuwa kwenye Kikao cha kuwawezesha Wabunge Wanawake juu ya Uelewa wa Utata na Uwiano usio sawa wa Mgawanyo wa Mirathi kwa Wajane na Wagane (Sheria zaMirathi) kwenye Ukumbi wa Msekwa Bunge Jijini Dodoma hii leo.
Sehemu ya Wabunge Wanawake wakifuatilia jambo kwenye Kikao cha kuwawezesha Wabunge Wanawake juu ya Uelewa wa Utata na Uwiano usio sawa wa Mgawanyo wa Mirathi kwa Wajane na Wagane (Sheria zaMirathi) kwenye Ukumbi wa Msekwa Bunge Jijini Dodoma hii leo.