WELCOME TO TANZANIA NATIONAL ASSEMBLY OFFICIAL BLOG: CONTACT US: P.O.BOX 941 DODOMA, TANZANIA, WEBSITE: parliament.go.tz , FIND US ON FACEBOOK >>> www.facebook.com/bungetz1, FOLLOW US ON TWITTER >>> @bunge_tz.>>>KARIBUNI

Thursday, March 3, 2016

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AFUNGUA SEMINA YA WABUNGE WA AFRIKA MASHARIKI .

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwahutubia Wabunge waliohudhuria Mkutano wa Wabunge wa Mabunge ya Afrika Mashariki baada ya kufungua Semina ya siku mbili (EALA) leo Jijini Dar es Salaam.



Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Job Ndugai akiwahutubia Wabunge waliohudhuria Mkutano wa Wabunge wa Mabunge ya Afrika Mashariki (EALA) leo Jijini Dar es Salaam.

Baadhi wa Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA) wakifuatilia hotuba za viongozi mbalimbali wakati wa Mkutano wa Wabunge wa Mabunge ya Afrika Mashariki (EALA) leo Jijini Dar es Salaam.


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan (mwenye ushungi) akiwa katika picha ya pamoja na Wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA) leo baada ya kufungua rasmi Semina ya siku mbili inayofanyika jijini Dar es Salaam.

(Picha zote na Benedict Liwenga)


Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan amefungua semina ya Wabunge wa Mabunge ya Afrika Mashariki (Inter-Parliamentary Relation Seminar -Nanyuki IX)  inayofanyika Jijini Dar es saalm kuanzia tarehe 2 hadi 4 Machi 2016 na kuwataka wabunge hao kuangalia kwa undani sheria zinazosimamia uchaguzi katika nchi za Afrika Mashariki ili kuondoa kasoro zinazojitokeza mara kwa mara.

Mhe. Samia amesema chaguzi nyingi zimekuwa na kasoro katika nchi za Afrika Mashariki hivyo mapendekezo yatakayopatikana katika mkutano huo yatasaidia kuwa na chaguzi huru na zinazofuata demokrasia katika mataifa ya Afrika Mashariki.

Kuhusu Uchaguzi wa Zanzibar Mhe. Samia amewahakikishia Wabunge hao kuwa hakutakuwa na vurugu na kwamba uchaguzi utakuwa huru na haki na kuwasihi Wazanzibari kuwa watulivu na kujitokeza kwa wingi kupiga kura.

Kwa upande wake Spika wa Bunge la Tanzania Mhe. Job Ndugai amesema amefurahi kuona mkutano huo umechagua suala la uchaguzi kuwa Dhima kuu  ya mkutano na kwamba anaamini kupitia mkutano huo kutapatikana mawazo mapya kwenye masuala ya demokrasia, utawala wa sheria, na uchaguzi.

Awali akimkaribisha Makamu wa Rais, Spika wa Bunge la Tanzania Mhe. Ndugai amesema huu ni wakati mzuri kujadili masuala ya uchaguzi kwa sababu baadhi ya nchi wanachama wametoka katika uchaguzi na kuwaomba wabunge hao kujadili kwa kina suala la uchaguzi na utamaduni wa kuachiana madaraka kwa amani ili kuepuka vurugu.

Naye Spika wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA) Mhe. Daniel Kidega amesema mkutano huo utaangalia namna ya kuboresha demokrasia katika nchi wanachama na kuangalia jinsi Mataifa ya Afrika Mashariki yanavyofuata sheria za kimataifa zinazohusu masuala ya uchaguzi.
Mhe. Kidega pia amewatakia wazanzibari uchaguzi mwema unaotarajia kufanyika hivi karibuni.

No comments:

Post a Comment