WELCOME TO TANZANIA NATIONAL ASSEMBLY OFFICIAL BLOG: CONTACT US: P.O.BOX 941 DODOMA, TANZANIA, WEBSITE: parliament.go.tz , FIND US ON FACEBOOK >>> www.facebook.com/bungetz1, FOLLOW US ON TWITTER >>> @bunge_tz.>>>KARIBUNI

Thursday, November 10, 2016

BUNGE KUFANYA KIKAO MAALUM CHA KUMUAGA ALIYEKUWA SPIKA WA BUNGE LA TISA MAREHEMU SITTA



BUNGE kesho litafanya Kikao Maalum cha Bunge kwa ajili ya kuuaga mwili wa Spika Mstaafu wa Bunge la Tisa, Mheshimiwa Samuel Sitta.
Akizungumzia kikao hicho Bungeni leo, Spika wa Bunge Mheshimiwa Job Ndugai alisema kikao hicho ni cha kihistoria na kwamba hakijawahi kutokea katika historia ya nchi.
Alisema mwili huo unataraijiwa kupokelewa na baadhi ya wabunge katika uwanja wa Ndege Mjini Dodoma majira ya saa 8 mchana na kuletwa Bungeni ambapo utaingizwa ndani ya Ukumbi wa Bunge.
“Wabunge mtapata nafsi ya kutoa salamu za rambirambi na baadaye kutakuwa na utaratibu maalum wa kutoa heshima za mwisho ambao tutaongozwa na Waziri Mkuu na Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni,” alisema.
Alisema kutokana na muda kuwa mchache hakutakuwa na zoezi la kuuga mwili mmoja mmoja na kwamba utaratibu uliondaliwa utaonyesha heshima kubwa kwa Spika huyo mstaafu.
“Tutajenga msingi mzuri ambao viongozi wetu wa kitaifa wakipatwa na jambo la namna hii watapata heshima hizo sio tu katika uwanja wa Taifa Dar es Salaam au mahali popote lakini kwa kuletwa Bungeni ambapo ndio nyumba ya wananchi wote wa Tanzania ilipo,” alisema.
Mheshimiwa Spika alisema baada ya shughuli hiyo kukamilika mwili wa marehemu utasindikizwa hadi Uwanja wa Ndege kwa ajili ya kusafirishwa kwenda Urambo Mkoani Tabora kwenye mazishi yanayotarajiwa kufanyika keshokutwa.
Alisema Bunge litawakilishwa na wabunge kumi watakaochaguliwa kwa kuzingatia uwakilishi wa vyama wakiongozwa na yeye mwenyewe.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Vijana, Kazi, Ajira na Watu wenye Ulemavu, Mheshimiwa Jenista Mhagama alitoa hoja ya kutengua Kanuni ili kikao hicho maalum cha kumuaga Marehemu Samuel Sitta kiweze kufanyika.





Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Job Ndugai akisaini Kitabu cha Maombolezo cha Msiba wa Spika Mstaafu wa Bunge la Tisa Marehemu Samuel Sitta Bungeni Mjini Dodoma

    Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Tulia Ackson akisaini Kitabu cha Maombolezo cha Msiba wa Spika Mstaafu wa Bunge la Tisa Marehemu Samuel Sitta Bungeni Mjini Dodoma.

Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Edwin Ambandusi Ngonyani Ndugai akisaini Kitabu cha Maombolezo cha Msiba wa Spika Mstaafu wa Bunge la Tisa Marehemu Samuel Sitta Bungeni Mjini Dodoma.

 Waheshimiwa Wabunge wakiendelea kusaini Kitabu cha Mambolezo cha Msiba wa Spika Mstaafu wa Bunge la Tisa Marehemu Samuel Sitta Bungeni Mjini Dodoma.

Add caption




No comments:

Post a Comment