Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kushoto) akikabidhiwa
Taarifa ya Kamati Maalum ya Kuchunguza Biashara ya Tanzanite na Mwenyekiti wa
Kamati hiyo Mhe. Dotto Biteko (kulia) katika tukio lililofanyika leo katika
Viwanja vya Bunge Mjini Dodoma. kushoto ni Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa na
Kulia ni Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Mhe. Freeman Mbowe
Mhe Zungu akizungumza wakati wa hafla hiyo
Naibu Spika Dkt Tulia Ackson akizungumza wakati wa hafla hiyo
Mhe Biteko akizungumza wakati wa hafla hiyo
Mhe Mbowe akizungumza wakati wa hafla hiyo
Mhe Spika akizungumza wakati wa hafla hiyo
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (wa pili kulia
waliokaa), Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa (wa pili kushoto waliokaa), Naibu
Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (kushoto waliokaa) na Kiongozi wa
Upinzani Bungeni, Mhe. Freeman Mbowe (kulia waliokaa) wakiwa katika picha ya
pamoja na Wajumbe wa Kamati Maalum ya Kuchunguza Biashara ya Almasi wakiongozwa
na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Mussa Azzan Zungu katika tukio lililofanyika leo
katika Viwanja vya Bunge Mjini Dodoma.
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (wa pili kulia
waliokaa), Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa (wa pili kushoto waliokaa), Naibu
Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (kushoto waliokaa) na Kiongozi wa
Upinzani Bungeni, Mhe. Freeman Mbowe (kulia waliokaa) wakiwa katika picha ya
pamoja na Wajumbe wa Kamati Maalum ya Kuchunguza Biashara ya Tanzanite wakiongozwa
na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Dotto Biteko katika tukio lililofanyika leo katika
Viwanja vya Bunge Mjini Dodoma.
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (wa pili kulia
waliokaa),Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa (wa pili kushoto waliokaa), Naibu
Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (kushoto waliokaa) na Kiongozi wa
Upinzani Bungeni, Mhe. Freeman Mbowe (kulia waliokaa) wakiwa katika picha ya
pamoja na Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kupokea
Taarifa ya Kamati Maalum ya Kuchunguza Biashara ya Almasi na Tanzanite katika
tukio lililofanyika leo katika Viwanja vya Bunge Mjini Dodoma.
Na Omary Machunda-Bunge
Spika
wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tazania Mhe Job Ndugai amepokea
taarifa za
Kamati maalum mbili alizounda wakati wa Mkutano wa Saba wa Bunge kwa
ajili ya kuchunguza juu ya mfumo bora wa uchimbaji, usimamizi,
umiliki na udhibiti wa biashara ya Madini ya Almasi na Tanzanite hapa
Nchini.
Aidha
mara baada ya kupokea ripoti hizo wakati wa hafla iliyofanyika katika viwanja
vya Bunge Mjini Dodoma, Mhe Ndugai alizikabidhi ripoti hizo kwa Waziri Mkuu wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Kassim Majaliwa kwa ajili ya utekelezaji.
Ripoti
ya uchunguzi wa Biashara ya Madini ya Alamsi iliwasilishwa na Mwenyekiti wa
Kamati hiyo Mhe Mussa Azzan Zungu wakati ripoti ya Kamati ya pili iliyochunguza
uchimbaji wa Madini ya Tanzanite iliwasilishwa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe
Dotto Biteko.
Akizungumza
mara baada ya kupokea ripoti hizo Spika Ndugai alisema kuwa mapambano ya kuhakikisha kuwa raslimali za Watanzania zinakuwa
mikononi mwao ni jambo la maana sana na hivyo; si vyema kumuachia Rais pekee
yake.
Kutokana na hilo Mhe Ndugai alisema kuwa Bunge kama mhimili lazima lijipambanue katika
kuhakikisha kuwa raslimali za nchi zinawanufaisha Watanzania wote.
“Hongereni
sana kwa kazi nzuri mliyoifanya, wakati mwingine mlikaa mpaka usiku wa manane,
mimi sina cha kuwalipa na wala Bunge hatuna cha kuwalipa bali mtalipwa na Mwenyezi
Mungu kwa kazi yenu nzuri mlioifanya kwa Taifa letu,” alisema.
“Wito wangu Watanzania wote tuwe
pamoja katika mapambano haya, lazima tuungane sote dhidi ya hao wanaotuumiza,”
alisema Mhe Ndugai.
Mhe Spika aliongeza kuwa baadhi
ya matatizo yamekuwa yakijurudia ikiwemo Mikataba mibovu ya uchimbaji madini, utendaji mbovu wa Bodi na mifumo mibuvo ya
kitaasisi zinazosimamia uchimbaji wa Madini.
“Ni lazima sasa tubadilike
kwa kuanza na upitiaji wa mikataba hiyo, upitiaji wa mifumo ya utendaji wa
taasisi zinazosimamia uchimbaji madini na kuwa makini katika uundaji wa bodi
mbalimbali,” Spika Ndugai alisisitiza.
Pia Mhe Ndugai, ameitaka Serikali kuyafanyia kazi
mapendekezo yote ya Kamati hizo na kusisitiza kuwa maoni yaliyowasilishwa ni
maoni ya Bunge zima na kwamba wataendeleza ushirikiano na Serikali
kuhakikisha wanawasidia Watanzania kufaidika na rasilimali za madini.
“Ni aibu sana kwa madini yanayopatikana nchini
mwetu pekee kunufaisha watu wa mataifa mengine na kuwaacha Watanzania katika
dimbwi la Umaskini” alisema.
Kwa upande wake Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim
Majaliwa aliahidi kuikabidhi kwa Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli mapema
kesho asubuhi na kwamba Serikali itayafanyia kazi mapendekezo yote ya Kamati
hizo haraka.
Awali
akizungumza kabla kukabidhi ripoti kwa Mhe Spika Mwenyekiti Mhe Zungu alisema
kuwa, katika utendaji wake Kamati imebaini
madudu mengi ikiwa ni pamoja na mikataba
mibovu wa uchimbaji madini,upotevu wa mapato, usimamizi mbovu wa uchimbaji wa
madini hayo, tofauti za kitwakwimu za uuzaji wa madini hayo nje ya nchi na
udanganyifu juu ya hali na gharama ya mitambo ya uchimbaji wa Madini ya Almasi.
Mhe
Zungu amesema ripoti imependekeza kuwa Serikali
iwahoji wajumbe wa bodi na wote wanaohusika na usimamizi wa uchimbaji wa madini
ya Almasi na ikibainikina kuwa
wamehusika na mapungufu yaliyoanishwa na ripoti basi wachukuliwe hatua.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati iliyoudwa
kuchunguza biashara ya Madini ya Tanzanite Mhe Dotto Biteko alisema pia
kumekuwa na usimamizi mbovu wa uchimbaji wa Madini hayo ya tanzanite, mikataba
mibovu, vitendo vya rushwa na udanganyifu katika biashara hiyo.
Kutokana
na hilo Mhe Biteko aliiomba Serikali kufanyia kazi mapendekezo ya Kamati ambayo
yatasaidia katika kuboresha uchimbaji wa
Tanzanite hapa nchini.
No comments:
Post a Comment