WELCOME TO TANZANIA NATIONAL ASSEMBLY OFFICIAL BLOG: CONTACT US: P.O.BOX 941 DODOMA, TANZANIA, WEBSITE: parliament.go.tz , FIND US ON FACEBOOK >>> www.facebook.com/bungetz1, FOLLOW US ON TWITTER >>> @bunge_tz.>>>KARIBUNI

Tuesday, November 24, 2020

SPIKA NDUGAI AWAAPISHA WABUNGE 19 WA VITI MAALUM WA CHADEMA JIJINI DODOMA

Wabunge Wateule wa Viti Maalum kutoka Chama cha Demokrasia na Maendeleo - CHADEMA wakisubiri kula kiapo kwenye viwanja vya Bunge Jijini Dodoma 

SPIKA wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai akimwapisha mbunge wa Viti Maalum CHADEMA Mheshimiwa Halima Mdee kwenye Viwanja vya Bunge Jijini Dodoma.

SPIKA wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai akimwapisha mbunge wa Viti Maalum CHADEMA Mheshimiwa Esther Matiko kwenye Viwanja vya Bunge Jijini Dodoma.

SPIKA wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai akimwapisha mbunge wa Viti Maalum CHADEMA Mheshimiwa Esther Bulaya kwenye Viwanja vya Bunge Jijini Dodoma.

SPIKA wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai akimwapisha mbunge wa Viti Maalum CHADEMA Mheshimiwa Cecilia Pareso kwenye Viwanja vya Bunge Jijini Dodoma.

Mbunge wa Viti Maalum CHADEMA Mheshimiwa Halima Mdee akiongea jambo kwa niaba ya Wabunge wengine wa CHADEMA walioapishwa katika  Viwanja vya Bunge Jijini Dodoma. 

SPIKA wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai na Katibu wa Bunge, Ndg. Stephen Kagaigai katika picha ya pamoja na Wabunge wa Viti Maalum CHADEMA mara baada ya kuwaapisha. 


Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai amewaapisha wabunge 19 wa viti maalum kutoka Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika viwanja vya Bunge Jijini Dodoma.

Akizungumza mara baada ya kuwaapisha, Spika wa Bunge alieleza utaratibu wa kikatiba uliotumika kuwapata wabunge hao pamoja na utaratibu wa kikanuni wa kuwaapisha katika kipindi ambacho hakuna Mkutano wa Bunge.

Aidha, aliwaahidi wabunge hao kuwalinda na kuwapa ushirikiano wa kila namna licha ya uchache wao Bungeni.

“Nawapongeza sana na mimi kama Spika jukumu langu ni kuwalinda walio wachache, hivyo naahidi kuwalinda na kuwapa ushirikiano wa kila hali wakati wa kutekeleza majukumu yenu,” alisema.

Akizungumza kwa niaba ya wabunge wenzake, Mheshimiwa Halima Mdee alimshukuru Spika kwa kuwapokea na kuahidi kufanya kazi kwa bidii kuwatumikia Watanzania.

Waheshimiwa Wabunge waliokula kiapo ni Halima Mdee, Grace Tendega, Esther Matiko, Cecilia Pareso, Esther Bulaya, Jesca Kishoa, Hawa Mwaifunga, Tunza Malapo, Naghenjwa Kaboyoka, Sophia Mwakagenda, Kunti Majala, Anatropia Theonest, Salome Makamba na Conchesta Rwamlaza.

 

Wengine ni Agnesta Kaiza, Nusrat Hanje, Asia Mohamed, Felister Njau na Stela Fiyao.

 

---------



No comments:

Post a Comment