WELCOME TO TANZANIA NATIONAL ASSEMBLY OFFICIAL BLOG: CONTACT US: P.O.BOX 941 DODOMA, TANZANIA, WEBSITE: parliament.go.tz , FIND US ON FACEBOOK >>> www.facebook.com/bungetz1, FOLLOW US ON TWITTER >>> @bunge_tz.>>>KARIBUNI

Sunday, March 14, 2021

KAMATI YA BUNGE YA ARDHI, MALIASILI NA UTALII YAIPONGEZA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII

 

Mratibu wa Mradi wa Panda Miti Kibiashara (PFP) Ndg. Rahel Swai akitoa taarifa na maelezo kuhusu mradi huo kwa Waheshimiwa wabunge kabla ya kufanya ziara na kuona mradi huo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii Mhe. Dkt. Aloyce Kwezi (mwenye scarf) kulia kwake Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (mb) Waziri wa Maliasili na Utalii wakiwaongoza wabunge kwenda kukagua Mradi wa Panda Miti kibiashara (PFP) Mafinga



Kamishna Uhifadhi wa TFS Prof. Dos Silayo akitoa taarifa kwa waheshimiwa wabunge ya Shamba la Miti Sao Hill kabla ya kufanya ukaguzi wa shamba hilo.


Na Zanele Chiza

Iringa.



Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii imeipongeza Wizara ya Maliasili na Utalii kupitia Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) kwa kupunguza tatizo la ujangili hapa nchini.

Mwenyekiti wa kamati hiyo Dkt. Aloyce Kwezi ametoa pongezi wakati wa ziara ya kamati hiyo katika Hifadhi ya Taifa ya Ruaha na maeneo yanayosimamiwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) ambapo amesema hatua hiyo imesaidia kwa kiasi kikubwa kuongezeka kwa idadi ya wanyama.

“Napongeza kazi kubwa iliyofanywa na Wizara, TANAPA wamefanya kazi kubwa sana ya kupunguza ujangili, hili limesaidia kuongezeka kwa idadi ya wanyamapori hapa nchini, pia nawapongeza TFS kwa kazi kubwa ambayo wamefanya” Amesema Dkt. Kwezi

Kuhusu uboreshaji wa miundombinu maeneo ya Hifadhi, Kamati hiyo imeishauri Wizara katika kipindi hiki cha bajeti kufuatilia kwa karibu ujenzi wa Barabara inayotoka Iringa kuelekea katika Hifadhi ya Taifa ya Ruaha.

No comments:

Post a Comment