Friday, October 20, 2023
Thursday, October 19, 2023
WAJUMBE WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MIUNDOMBINU WAPOKEA NA KUJADILI TAARIFA YA WIZARA YA UJENZI KUHUSU UTENDAJI WA WAKALA WA MAJENGO TANZANIA (TBA).
Wajumbe wa kamati
ya kudumu ya Bunge ya Miundombinu wakiongozwa na Mwenyekiti wa kamati hiyo,
Mhe. Selemani Kakoso wamepokea na kujadili taarifa ya Wizara ya Ujenzi kuhusu
utendaji wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kwa kipindi cha Julai - Oktoba,
2023; Mafanikio na Changamoto katika kikao kilichofanyika leo tarehe 19 Oktoba,
2023 katika ofisi za Bunge Jijini Dodoma.
Aidha, kikao hicho
kimehudhuriwa na Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhe. Godfrey Kasekenya, Katibu Mkuu wa
Wizara ya Ujenzi, Mhe. Balozi Aisha Amour na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo
Tanzania (TBA), Arch. Daud Kondoro.
Saturday, October 7, 2023
Tuesday, October 3, 2023
TIMU ZA BUNGE ZAENDELEA KUFANYA VIZURI KATIKA MICHEZO YA SHIMIWI MKOANI IRINGA
Timu
za Klabu ya michezo za Bunge zimeendelea kufanya vizuri katika michezo ya
Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI) inayoendelea leo
tarehe 3 Oktoba Mkoani Iringa.
Timu
ya kamba wanawake imeigaragaza timu ya Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo
kwa pointi 2-0 huku timu ya kamba wanaume ikiiburuza timu ya Ujenzi kwa pointi
1-0 wakati wa mchezo uliofanyika katika viwanja vya Chuo Kikuu Kishiriki cha
Elimu Mkwawa.
Nayo
timu ya netiboli imeibuka kidedea baada ya kuibugiza magoli 31 - 16 timu ya
Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum wakati wa
mchezo uliofanyika katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Ruaha (RUCU).
Kwa
upande wa timu ya soka ya Bunge imeicharaza goli 2 -1 timu ya soka ya Wizara ya
Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa wakati wa mchezo uliofanyika katika uwanja wa CCM
Samora Mkoani hapa.
Michezo
SHIMIWI inaendelea kutimua vumbi Katika viwanja mbalimbali na inategemewa
kuhitimishwa tarehe 14 Oktoba, 2023, Mkoani Iringa.
Saturday, September 2, 2023
MATUKIO KATIKA PICHA YALIYOJIRI WAKATI WA NMB BUNGE BONANZA
Matukio katika
picha yaliyojiri wakati wa NMB Bunge Bonanza
katika michezo ya Mpira wa Wavu, Kurusha Tufe, Karata, Draft na Pool
Table leo tarehe 2 Septemba, 2023 katika viwanja vya Shule ya Sekondari John
Merlin, Jijini Dodoma.
Katika michezo
hiyo, mgeni rasmi alikuwa ni Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mhe.
Zubeir Ali Maulid.







