WELCOME TO TANZANIA NATIONAL ASSEMBLY OFFICIAL BLOG: CONTACT US: P.O.BOX 941 DODOMA, TANZANIA, WEBSITE: parliament.go.tz , FIND US ON FACEBOOK >>> www.facebook.com/bungetz1, FOLLOW US ON TWITTER >>> @bunge_tz.>>>KARIBUNI

Wednesday, May 24, 2017

MHE SPIKA ATEMBELEA BUNGE LA KENYA

 
    Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Job Ndugai  (wa pili kushoto) akisikiliza maelezo kuhusu Bunge la Kenya linavyofanya kazi kutoka kwa Spika wa Bunge hilo Mhe Justin Muturi.Mhe Ndugai yuko katika ziara ya kibunge nchini Kenya kwa mwaliko Bunge la Kenya ambapo amembatana na wajumbe wa Tume ya Utumishi ya Bunge, Mhe Mary Chatanda, Mhe Salim Turky na Mhe Mch.Peter Msigwa.



Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Job akipokea zawadi kutoka Spika wa Bunge la Kenya Mhe Justin Muturi.   



Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Job Ndugai yuko katika ziara ya kibunge nchini Kenya kwa mwaliko wa Spika wa Bunge la Kenya Mhe Justin Muturi ambapo amembatana na wajumbe wa Tume ya Utumishi ya Bunge,Mhe Mary Chatanda,Mhe Salim Turky na Mhe Mch.Peter Msigwa.
Aidha akizungumza alipokutana na Spika Wa Bunge la Kenya Mhe Ndugai amesema kuwa alipokea mwaliko wa kutembelea Bunge la Kenya kutoka na historia kubwa ambayo mabunge yote mawili yanao.
"Mabunge yetu mawili yamekuwa na ushirikiano mkubwa kwa miaka mingi," alisema Mhe Ndugai.
Kwa upande wake Spika Wa Bunge la Kenya Mhe Muturi alisema "tumefurahi kwa kukubali mwaliko wetu na kuambatana na wabunge.Kupitia ziara yako nina imani sote wawili tutajifunza mengi katika uendeshaji Bunge hususan kwa mabadiliko ambayo hapa Kenya tumefanya".


No comments:

Post a Comment