WELCOME TO TANZANIA NATIONAL ASSEMBLY OFFICIAL BLOG: CONTACT US: P.O.BOX 941 DODOMA, TANZANIA, WEBSITE: parliament.go.tz , FIND US ON FACEBOOK >>> www.facebook.com/bungetz1, FOLLOW US ON TWITTER >>> @bunge_tz.>>>KARIBUNI

Friday, October 20, 2017

SPIKA NDUGAI KATIKA MKUTANO WA 137 WA CHAMA CHA MABUNGE DUNIANI JIJINI ST. PETERSBURG, URUSI



Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto)akizungumza  na Spika wa Bunge la Kuwait, Mheshimiwa Marzouq Al Ghanim (kulia) kabla ya kuanza kwa Mkutano Mkuu wa 137 wa Umoja wa Mabunge Duniani uliofanyika leo katika Jiji la  St. Petersburg, Urusi. Kushoto kwake ni Mbunge wa Kigoma kaskazini, Mheshimiwa Peter Serukamba na anaefuata ni Katibu wa Spika, Ndg. Said Yakubu



Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (wa pili kushoto)akizungumza  na Spika wa Bunge la Burundi, Mheshimiwa Pasc Nyabenda (wa pili kulia) kabla ya kuanza kwa Mkutano Mkuu wa 137 wa Umoja wa Mabunge Duniani uliofanyika leo katika Jiji la St. Petersburg, Urusi.


Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (wa pili kushoto) akipokea zawadi kutoka kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Ndg. Martin Chungong (kushoto) alipomtembelea ofisini kwake wakati wa Mkutano wa 137 wa Umoja wa Mabunge Duniani unaoendelea Jijini St. Petersburg, Urusi



Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai akipiga kura ya kumchagua Rais wa Chama cha Mabunge Duniani (IPU) wakati wa Mkutano wa 137 wa Umoja wa Chama cha Mabunge Duniani unaoendelea Jijini St Petersburg,Urusi. Nyuma yake ni Mbunge wa Kigoma kaskazini, Mheshimiwa Peter Serukamba na Mbunge wa Viti Maalum Mheshimiwa Susan Lyimo.






Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (wa pili kulia)katika mazungumzo na Kiongozi wa Chama cha Kikomunisti cha Urusi na kiongozi wa Bunge la nchi hiyo, Komredi Gennady Zyuganov (wa pili kushoto) alipomtembelea leo ofisini kwake katika maadhimisho ya miaka 100 ya Mapinduzi Makuu ya Urusi. Mheshimiwa Spika yupo nchini Urusi, akishiriki Mkutano wa 137 wa Chama cha Mabunge Duniani unaoendelea leo Jijini St. Petersburg, Urusi
 



Spika wa Bunge Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) akimkabidhi zawadi Kiongozi wa Chama cha Kikomunisti cha Urusi na kiongozi wa Bunge la nchi hiyo Komredi Gennady Zyuganov (katikati) alipomtembelea ofisini kwake. Kulia ni Balozi wa Tanzania nchini huko, Jenerali Mstaafu Wynjones kisamba. Mheshimiwa Spika yupo nchini humo kushiriki mkutano wa 137 wa Chama cha Mabunge Duniani.




Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) akivishwa nishani maalum ya maadhimisho ya miaka 100 ya Mapinduzi Makuu ya Urusi na Kiongozi wa Chama cha kikomunisti cha Urusi, Komredi Gennady Zyuganov ambae ni Kiongozi wa Chama cha Kikomunisti cha Urusi na kiongozi wa Bunge la nchi hiyo alipomtembelea ofisini kwake. Mheshimiwa Spika yupo nchini humo akishiriki Mkutano wa 137 wa Chama cha Mabunge Duniani.

No comments:

Post a Comment