WELCOME TO TANZANIA NATIONAL ASSEMBLY OFFICIAL BLOG: CONTACT US: P.O.BOX 941 DODOMA, TANZANIA, WEBSITE: parliament.go.tz , FIND US ON FACEBOOK >>> www.facebook.com/bungetz1, FOLLOW US ON TWITTER >>> @bunge_tz.>>>KARIBUNI

Friday, October 19, 2018

SPIKA WA BUNGE AKUTANA NA UJUMBE KUTOKA BUNGE LA CHINA


Spika wa Bunge Mheshimiwa Job Ndugai akizungumza na Mgeni wake Mheshimiwa Prof. Lou Jiwei ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kamati ya Mambo ya Nje ya Bunge la China (CPPCC) alipomtembelea hii leo na kufanya nae mazungumzo kwenye Ukumbi wa Spika Jijini Dodoma.
Spika wa Bunge Mheshimiwa Job Ndugai akimvalisha vazi la Kimasai mgeni wake ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kamati ya Mambo ya Nje ya Bunge la China (CPPCC) Mheshimiwa Prof. Lou Jiwei kama ishara ya Utamaduni wa Kitanzania walipokutana na kufanya mazungumzo kwenye Ukumbi wa Spika Jijini Dodoma hii leo.
Spika wa Bunge Mheshimiwa Job Ndugai akisalimiana na Balozi wa China hapa nchini Mheshimiwa Wang Ke alipomtembelea na kufanya nae mazungumzo hii leo kwenye Ukumbi wa Spika Jijini Dodoma. Balozi huyo aliambatana na ujumbe kutoka Bunge la China ulioongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Kamati ya Mambo ya Nje ya Bunge la China (CPPCC) Mheshimiwa Prof. Lou Jiwei.
Spika wa Bunge Mheshimiwa Job Ndugai akiwa katika picha ya pamoja na Wageni kutoka China wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Kamati ya Mambo ya Nje ya Bunge la China (CPPCC) Mheshimiwa Prof. Lou Jiwei (kulia kwa Spika) walipokutana hii leo kwenye Ukumbi wa Spika Jijini Dodoma, kushoto kwa Spika ni Balozi wa China hapa nchini Mheshimiwa Wang Ke. Baadhi ni Watumishi wa Ofisi ya Bunge.
Wageni wa Mheshimiwa Spika kutoka nchini China wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Kamati ya Mambo ya Nje ya Bunge la China (CPPCC) Mheshimiwa Prof. Lou Jiwei wakipewa maelekezo kuhusiana na mpangilio wa ukaaji Bungeni kutoka kwa Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Itifaki na Uhusiano wa Kimataifa – Ofisi ya Bunge, Ndg. Daniel Eliufoo walipotembelea Bungeni Jijini Dodoma hii leo.


No comments:

Post a Comment