WELCOME TO TANZANIA NATIONAL ASSEMBLY OFFICIAL BLOG: CONTACT US: P.O.BOX 941 DODOMA, TANZANIA, WEBSITE: parliament.go.tz , FIND US ON FACEBOOK >>> www.facebook.com/bungetz1, FOLLOW US ON TWITTER >>> @bunge_tz.>>>KARIBUNI

Thursday, November 12, 2020

BUNGE LAMTHIBITISHA MHE. KASSIM MAJALIWA KUWA WAZIRI MKUU

Mpambe wa Rais akiingia Bungeni kuwasilisha bahasha yenye Jina la Waziri Mkuu aliyeteuliwa na Mhe. Rais kwa ajili ya kudhibitishwa na Bunge.

Spika wa Bunge, Mhe. Job Y. Ndugai akionesha kwa Waheshimiwa Wabunge bahasha yenye Jina la Waziri Mkuu mara baada ya kuipokea kutoka kwa Mpambe wa Rais.

Spika wa Bunge, Mhe. Job Y. Ndugai (kulia) na Katibu wa Bunge, Stephen Kagaigai (katikati) wakifungua bahasha yenye Jina la Waziri Mkuu kutoka kwa Mheshimiwa Rais. Kushoto ni Mpambe wa Rais.

Spika wa Bunge, Mhe. Job Y. Ndugai (kulia) akitangaza  Jina la Waziri Mkuu mara baada ya kupokea bahasha yenye jina hilo kutoka kwa Mhe. Rais.

Mbunge wa Ruangwa, Mhe. Kassim Majaliwa akipongezwa na Waheshimiwa Wabunge mara baada ya kutangazwa  kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mbunge wa Ruangwa, Mhe. Kassim Majaliwa akipongezwa na Waheshimiwa Wabunge mara baada ya kutangazwa  kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


 Mbunge wa Ruangwa, Mhe. Kassim Majaliwa akipongezwa na Waheshimiwa Wabunge mara baada ya kutangazwa  kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

 

Mbunge wa Ruangwa, Mhe. Kassim Majaliwa akizungumza mara baada ya kudhibitishwa na Wabunge kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

 Bunge limemthibitisha Mbunge wa Jimbo la Ruangwa mkoani Lindi, Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa kuwa Waziri Mkuu kwa miaka mitano mingine (2020-2025) kwa kupata kura zote 350 zilizopigwa na wabunge sawa na asilimia 100.

    Akitangaza matokeo ya kura, Spika wa Bunge, Job Ndugai alisema katika ya kura zote 350 zilizopigwa hakukuwa na kura ya hapana wala kura iliyoharibika.

    “Kura zote zilizopigwa ni 350 hakuna iliyoharibika, hakuna kura ya hapana. Kura zote 350 zimemthibitisha Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa, kwa hiyo ndugu wabunge Mheshimiwa Majaliwa amethibitishwa na Bunge hili kuwa Waziri Mkuu kwa kura 350 sawa na asilimia 100.

    Awali jina la Waziri Mkuu mteule liliwasilishwa Bungeni na Mpambe wa Rais na kukabidhiwa kwa Mheshimiwa Spika.

    Akizungumza baada ya kuthibitishwa Mheshimiwa Majaliwa amesema amepokea uteuzi huo kwa mikono miwili na anamshukuru Mwenyezi Mungu ambaye ameendelea kuwapa uhai wote na kushuhudia hayo, Pia amemshukuru Rais Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kwa imani kubwa aliyoionesha juu yake.

    “Mheshimiwa Spika jambo hili si dogo, Mwenyezi Mungu ameliongoza, namshukuru Mheshimiwa Rais Dkt John Pombe Magufuli kwa imani kubwa aliyonayo juu yangu na kuendelea kuniamini. Namshukuru sana na Makamu wa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa ushiriki wake katika kuridhia jina langu.” Alisema.

    Mheshimiwa Majaliwa alimpongeza pia Mheshimiwa Spika kwa kuchaguliwa bila kupingwa kuwa mbunge wa Kongwa pamoja na kurudi katika nafasi yake ya uspika baada ya kupigiwa kura nyingi na waheshimiwa wabunge.

    Awali kabla ya kuthibitisha jina la Waziri Mkuu wabunge mbalimbali walizungumzia utendaji kazi wa Mheshimwa Majaliwa ambapo Mbunge wa Tunduma, Mheshimiwa David Silinde alitumia fursa hiyo kumpongeza Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kumrudisha tena Waziri Mkuu Kassim Majaliwa katika nafasi hiyo.

    Wabunge wengine waliopata fursa ya kumpongeza na kuzungumzia utendaji wake ni pamoja na Mheshimiwa William Lukuvi, Mheshimiwa Kapten Mstaafu George Mkuchika, Mheshimiwa Mama Salma Kikwete, Mheshimiwa Fakharia Shomari na Mheshimiwa Januari Makamba.

 

No comments:

Post a Comment