WELCOME TO TANZANIA NATIONAL ASSEMBLY OFFICIAL BLOG: CONTACT US: P.O.BOX 941 DODOMA, TANZANIA, WEBSITE: parliament.go.tz , FIND US ON FACEBOOK >>> www.facebook.com/bungetz1, FOLLOW US ON TWITTER >>> @bunge_tz.>>>KARIBUNI

Thursday, November 12, 2020

DKT. TULIA ACHAGULIWA KUWA SPIKA WA BUNGE LA 12

Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Mhe. Dkt. Tulia Ackson akiapa mara baada ya kuchaguliwa kuwa Naibu Spika wa Bunge la 12, Jijini Dodoma.
Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Mhe. Dkt. Tulia Ackson akizungumza mara baada ya kuchaguliwa kuwa Naibu Spika wa Bunge la 12, Bungeni Dodoma.

   

 Bunge limechagua Mheshimiwa Dkt. Tulia Ackson kuwa Naibu Spika wa Bunge la 12.

Akitangaza matokeo hayo mara baada ya uchaguzi kufanyika, Spika wa Bunge Mheshimiwa Job Ndugai alisema Dkt. Tulia amepata kura 350 kati ya kura 354 zilizopigwa.

Akizungumza mara baada ya kutangazwa mshindi, aliwashukuru Wabunge wote kwa ushindi huo wa kishindo na kuahidi kufanya nao kazi bega kwa bega bila kujali tofauti za kisiasa.

“Naahadi nitawatumikia, nitafanya kazi kwa ufanisi katika kazi zangu kama Naibu Spika, msisite kuniletea hoja zenu pale mnapukuwa nazo,” alisema

Aidha, alisema atamshauri vizuri Spika juu ya Sheria na Kanuni kwa kutumkia uzoefu alionao ili kuhakikisha haki inatendeka kwa wote.

 

 


No comments:

Post a Comment