WELCOME TO TANZANIA NATIONAL ASSEMBLY OFFICIAL BLOG: CONTACT US: P.O.BOX 941 DODOMA, TANZANIA, WEBSITE: parliament.go.tz , FIND US ON FACEBOOK >>> www.facebook.com/bungetz1, FOLLOW US ON TWITTER >>> @bunge_tz.>>>KARIBUNI

Friday, August 16, 2019

KAMATI YA PAC YAPEWA MAFUNZO NA OFISI YA MSAJILI WA HAZINA

Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali PAC wakifuatilia jambo kwa karibu kwenye Semina kuhusu Changamoto za usimamizi wa matumizi ya Mashirika ya Umma nchini iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Msekwa Bungeni Jijini Dodoma hii leo. 
Mkurugenzi wa Uwekezaji kutoka Ofisi ya Msajili wa Hazina Ndg. Lightness Mauki akifafanua jambo alipokuwa akitoa Mada kuhusu Changamoto za usimamizi wa Matumizi ya Mashirika ya Umma nchini kwa wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali PAC iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Msekwa Bungeni Jijini Dodoma hii leo. 


Thursday, August 15, 2019

BARAZA LA WAFANYAKAZI WA OFISI YA BUNGE LANDELEA NA KIKAO

Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Bunge, Ndugu Stephen Kagaigai akizungumza katika kikao kilichofanyika katika Ofisi  Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar, pamoja naye ni Katibu wa Baraza Ndugu Frank Mbilinyi.

Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Bunge, Ndugu Stephen Kagaigai akizungumza katika kikao kilichofanyika katika Ofisi  Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar, pamoja naye ni Katibu wa Baraza Ndugu Frank Mbilinyi.
Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Afya na Serikali Kuu (TUGHE), Tawi la Bunge, Ndugu Chacha Nyakega akitoa nasaha za chama hicho katika kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Bunge lililofanyika katika Ofisi ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar.

Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Afya na Serikali Kuu (TUGHE), Tawi la Bunge, Ndugu Chacha Nyakega akitoa nasaha za chama hicho katika kikao cha Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Bunge lililofanyika katika Ofisi ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar.
Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Bunge wakifuatilia mada kuhusu Umuhimu wa Kuzingatia Maadili katika Utumishi wa Umma katika shughuli za Bunge kilichofanyika Ofisi Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar

Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Bunge wakifuatilia mada kuhusu Umuhimu wa Kuzingatia Maadili katika Utumishi wa Umma katika shughuli za Bunge kilichofanyika Ofisi Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar



Wednesday, August 14, 2019

SPIKA WA BUNGE AWATAKA WAFANYAKAZI WA OFISI YA BUNGE KUFANYA KAZI KWA BIDII




Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai amewataka watumishi wa Bunge kuacha kufanya kazi kwa mazoea badala yake wafanye kazi kwa bidii.

Mhe. Spika alitoa rai hiyo kupitia hotuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Naibu Spika, Mhe. Dkt. Tulia Ackson alipokuwa anazindua Baraza la Wafanyazi la Ofisi ya Bunge lililofanyika  katika Ofisi Ndogo za Bunge Tunguu Zanzibar.

Alisema kunahitajika mabadiliko katika utekelekezaji wa majukumu ya kila siku kwa watumishi katika kuchapa kazi ili kuleta utendaji kazi wenye tija na ufanisi.

Aidha, aliwataka wajumbe kupitia mada zitakazowasilishwa katika Mkutano huo wa Baraza kukumbuka wajibu wao katika kutelekeza majukumu waliyopewa kulingana na taaluma husika na hatimaye kufanikisha utekelezaji bora wa majukumu na madaraka ya Bunge Kikatiba.

Vilevile, alimpongeza Katibu wa Bunge, Ndugu Stephen Kagaigai kwa kufanikisha utatuzi wa changamoto ya muda mrefu ya muundo wa Ofisi ya Bunge ambayo hatimaye ufumbuzi umewezesha kuundwa kwa Baraza la Wafanyakazi.

“Naomba nitumie fursa hii kuwapongeza watumishi wote mlioteuliwa na Tume ya Utumishi wa Bunge kushika nyadhifa mbalimbali za uongozi na ni matumini yangu kwamba mtatumia uwezo na karama mlizojaaliwa na Mwenyezi Mungu katika kutekeleza majukumu yenu kwa ufanisi hivyo kuliwezesha Bunge kufikia malengo yake,” alisema.

Aliwapongeza pia Wajumbe na Wawakilishi wa Idara na Vitengo kwa kuchaguliwa kushika nafasi hizo na kuwataka kutumia nafasi zao ili kuwa kiungo kati ya Wafanyakazi wa kada, ngazi zote, Menejimenti na Tume ya Utumishi wa Bunge.

Uzinduzi wa Baraza la Wafanyakazi ulihudhuriwa na Katibu Mkuu Taifa wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya, TUGHE Ndugu Hery Nkunda na Katibu wa TUGHE Mkoa wa Dodoma Ndugu John Mchenya ambao walinasihi Baraza kudumisha ushirikiano na kuongeza ufanisi katika ujenzi wa nchi.

Awali akizungumza katika mkutano huo, Katibu wa Bunge Ndugu Stephen Kagaigai alisema Ofisi ya Bunge imeunda Baraza la Wafanyakazi baada kutokuwepo ya Baraza hilo katika kipindi kirefu kutokana na changamoto zilizokuwepo za kimuundo za Ofisi ya Bunge.

Alisema, lengo la Baraza lililopo kisheria ni kuboresha utendaji kazi  wa taasisi kwa kufanya kazi kwa ushirikiano na bila ya ugomvi  wala mifarakano.

Kabla ya uzinduzi wa Baraza la Wafanyakazi, wajumbe walimchagua Ndugu Frank Mbilinyi kuwa katibu wa Baraza na Ndugu Felister  Njovu kuwa Katibu Msaidizi.



NAIBU SPIKA AZINDUA BARAZA LA WAFANYAKAZI OFISI YA BUNGE

Katibu wa Bunge, Ndugu Stephen Kagaigai (katikati) akiimba wimbo wa mshikamano wa Wafanyakazi kabla ya kuanza kwa Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi la  Ofisi ya Bunge uliofanyika katika Ofisi Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar pamoja na Ndugu Chacha Nyakega Mwenyekiti wa  TUGHE Tawi la Ofisi ya Bunge na Ndugu Triphonia Mng’ong’o Kaimu Mkurugenzi  wa Idara ya  Utawala na  Rasilimaliwatu.

Naibu Spika wa Bunge la Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson akifungua Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi la  Ofisi ya Bunge uliofanyika katika Ofisi Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar

Naibu Spika wa Bunge la Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson akifungua Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi la  Ofisi ya Bunge uliofanyika katika Ofisi Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar

Naibu Spika wa Bunge la Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson akimkabidhi Katibu wa Bunge, Ndugu Stephen Kagaigai Mkataba kwa ajili ya kuunda Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Bunge mara baada ya kuzindua Baraza hilo. Uzinduzi huo umefanyika katika Ofisi Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar


Naibu Spika wa Bunge la Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson akimkabidhi Katibu Mkuu wa TUGHE Taifa, Ndugu Hery Nkunda Mkataba kwa ajili ya kuunda Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Bunge baada ya uzinduzi. Uzinduzi huo umefanyika katika Ofisi Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar
Naibu Spika wa Bunge la Tanzania, Mhe. Dkt. Tulia Ackson akimkabidhi Katibu Mkuu wa TUGHE Mkoa wa Dodoma , Ndugu John Mchenya  Mkataba kwa ajili ya kuunda Baraza la Wafanyakazi la Ofisi ya Bunge mara baada ya kuzindua Baraza hilo. Uzinduzi huo umefanyika katika Ofisi Ndogo za Bunge, Tunguu Zanzibar
 
Wajumbe wa Baraza wakiwa katika picha ya pamoja



Friday, August 9, 2019

WAGENI MBALIMBALI WATEMBELEA BANDA LA BUNGE KWENYE MAONESHO YA NANENANE JIJINI DODOMA

Wanafunzi wa Shule ya Awali na Msingi Modern ya Jijini Dodoma wakifurahia Siwa wakati walipotembelea banda la Bunge kwenye Maonesho ya Wakulima ya Nanenane Jijini Dodoma hii leo. Kushoto ni Afisa Utafiti wa Ofisi ya Bunge Ndg. Aziza Makwai akiwasaidia Wanafunzi hao namna ya kubeba Siwa.

Afisa wa Bunge Ndg. Hosiana John akitoa Elimu kwa mgeni aliyetembelea banda la Bunge hii leo kwenye Maonesho ya Wakulima ya Nanenane yanayoendelea Jijini Dodoma.

Afisa wa Bunge Ndg. Mohamed Salim akitoa Elimu kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari Dodoma walipotembelea banda la Bunge kwenye Maonesho ya Wakulima ya Nanenane Jijini Dodoma hii leo.