WELCOME TO TANZANIA NATIONAL ASSEMBLY OFFICIAL BLOG: CONTACT US: P.O.BOX 941 DODOMA, TANZANIA, WEBSITE: parliament.go.tz , FIND US ON FACEBOOK >>> www.facebook.com/bungetz1, FOLLOW US ON TWITTER >>> @bunge_tz.>>>KARIBUNI

Thursday, March 30, 2017

KAMATI YA MIUNDOMBINU YAJADILI BAJETI YA WIZARA YA UJENZI

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu wakiwa katika kikao ambapo leo wamepokea Taarifa
kuhusu utekelezaji wa bajeti ya Mwaka wa Fedha 2016/17 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2017/18  ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu wakifuatilia mjadala katika kikao hicho ambapo leo wamepokea Taarifa kuhusu utekelezaji wa bajeti ya Mwaka wa Fedha 2016/17 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2017/18  ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

KAMATI YAJADILI BAJETI YA MKOA WA ARUSHA

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Utawala na Serikali za Mitaa , Mhe. Venance Mwamoto akisikiliza  taarifa kuhusu utekelezaji wa bajeti ya Mwaka wa Fedha 2016/17 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2017/18 ya Ofisi ya Rais TAMISEMI, fungu namba 70 Mkoa wa Arusha, kushoto ni Katibu wa Kamati hiyo Ndg. Chacha Nyakega


Wajumbe wa Kamati ya Utawala na Serikali za Mitaa wakifuatilia uwasilishwaji wa  taarifa kuhusu utekelezaji wa bajeti ya Mwaka wa Fedha 2016/17 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2017/18 ya Ofisi ya Rais TAMISEMI, fungu namba 70 Mkoa wa Arusha.


Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mhe. Seleman Jafo akifiuatilia mjadala kuhusiana na taarifa kuhusu utekelezaji wa bajeti ya Mwaka wa Fedha 2016/17 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2017/18 ya Ofisi ya Rais TAMISEMI, fungu namba 70 Mkoa wa Arusha katika kikao cha Kamati ya Utawala na Serikali za Mitaa.Kushoto ni viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Arusha


Mjumbe wa Kamati Utawala na Serikali za Mitaa  Mhe. Juma Ngwali akisisitiza jambo katika kikao cha kamati hiyo ambacho kilipokea taarifa kuhusu utekelezaji wa bajeti ya Mwaka wa Fedha 2016/17 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2017/18 ya Ofisi ya Rais TAMISEMI, fungu namba 70 Mkoa wa Arusha.

KAMATI YA ARDHI, MALIASILI NA UTALII YAENDELEA NA UCHAMBUZI WA BAJETI

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii  Mhe. Mary Chatanda na Mhe. Silafu Maufi wakifuatilia uwasilishwaji wa Taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti ya Wizara ya Maliasili na Utalii katika kikao cha Kamati hiyo.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe akiwasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti ya Wizara yake kwa Mwaka wa Fedha 2016/17 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka ujao wa fedha mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii.

KAMATI YA MAMBO YA NJE, ULINZI NA USALAMA YAJADILI BAJETI YA WIZARA YA MAMBO NDANI YA NCHI

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba akiwasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti ya Wizara yake kwa mwaka 2016/17 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka ujao wa fedha mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, kulia ni Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Balozi Adadi Rajabu.

Viongozi mbalimbali kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi wakifuatilia uwasilishwaji wa Taarifa ya Utekelezaji wa Bajeti ya Wizara hiyo ya kwa mwaka 2016/17 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka ujao wa fedha mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama.