WELCOME TO TANZANIA NATIONAL ASSEMBLY OFFICIAL BLOG: CONTACT US: P.O.BOX 941 DODOMA, TANZANIA, WEBSITE: parliament.go.tz , FIND US ON FACEBOOK >>> www.facebook.com/bungetz1, FOLLOW US ON TWITTER >>> @bunge_tz.>>>KARIBUNI

Thursday, August 13, 2020

WATUMISHI WA KITENGO CHA TEHAMA WAPEWA MAFUNZO KUHUSU MFUMO WA KADI YA TATHIMINI NA UWAJIBIKAJI WA MALARIA



Watumishi wa Kitengo cha TEHAMA wa Ofisi ya Bunge wakipatiwa mafunzo kuhusu mfumo wa Kadi ya Tathimini na Uwajibikaji wa Malaria kutoka kwa Ndugu Khalifa Munisi. Mafunzo hayo yameandaliwa na Umoja wa Wabunge walio katika Mapambano dhidi ya Malaria (TAPAMA) kwa kushirikiana na Wizara ya Afya kupitia Programu ya Taifa ya Kupambana na Kutokomeza Malaria pamoja na Sekretarieti ya Maraisi na Viongozi wa Afrika walioungana kupambana na Malaria. Lengo la kuwajengea uwezo watumishi wa kitengo hicho ili waweze kuiwasaidia wabunge kutumia Kadi hiyo kupitia kwenye vishikwambi (‘tablet’) vyao.

Mafunzo yakiendelea katika Ukumbi wa Msekwa B

Mafunzo yakiendelea


 

Tuesday, July 7, 2020

WANANCHI WENGI WAVUTIWA NA BANDA LA BUNGE MAONYESHO YA SABASABA

Afisa Mwandamizi wa Bunge Ndg. Louise Mdachi akitoa Elimu kwa wageni mbalimbali waliofika kutembelea Banda la Bunge kwenye Maonyesho ya Sabasaba Jijini Dar Es Salaam hii leo. 

Afisa wa Bunge Ndg. Peter Magati akitoa Elimu kwa wageni mbalimbali waliofika kutembelea Banda la Bunge kwenye Maonyesho ya Sabasaba Jijini Dar Es Salaam hii leo.

Afisa wa Bunge Ndg. Rehema Kipera akitoa Elimu kwa wageni mbalimbali waliofika kutembelea Banda la Bunge kwenye Maonyesho ya Sabasaba Jijini Dar Es Salaam hii leo.

Sunday, July 5, 2020

WANANCHI MBALIMBALI WAENDELEA KUTEMBELEA BANDA LA BUNGE SABASABA

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na  Ushirikiano wa Kimataifa Dkt. Damas Ndumbalo akisaini Kitabu cha Mahudhurio ya Wageni Mahsusi wanatembelea Banda la Bunge ili kupata Elimu kuhusiana Shughuli za Mhimili huu wa Kutunga Sheria. 

Afisa wa Bunge Ndg. Amina Salum akitoa ufafanuzi kwa Wageni mbalimbali wanaofika kwenye Banda la Bunge ili kupata Elimu kuhusiana Shughuli za Mhimili huu wa Kutunga Sheria. 

Afisa wa Bunge Ndg. Katherine Kaihula akitoa ufafanuzi kwa Wageni mbalimbali wanaofika kwenye Banda la Bunge ili kupata Elimu kuhusiana Shughuli za Mhimili huu wa Kutunga Sheria. 

Afisa wa Bunge Ndg. Zanele Chiza akifafanua jambo kwa Wageni mbalimbali wanaofika kwenye Banda la Bunge ili kupata Elimu kuhusiana Shughuli za Mhimili huu wa Kutunga Sheria. 

Sunday, June 28, 2020

SPIKA AKABIDHI KOMPYUTA 20 SHULE ZA SEKONDARI WILAYA YA KONGWA

Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akizungumza hafla ya makabidhiano ya Kompyuta 20 alizozitoa kwa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa kwa ajili ya shule za sekondari za Wilaya hiyo, kushoto ni Mkurugenzi wa Elimu TAMISEMI, Ndugu Julius Nestory na kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kongwa aliyemaliza muda wake Ndugu White Zuberi.Hafla hiyo imefanyika katika Ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa.

Mkurugenzi wa Elimu TAMISEMI, Ndugu Julius Nestory akizungumza katika hafla ya makabidhiano ya Kompyuta 20 zilizotolewa na Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai kwa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa kwa ajili ya shule za sekondari za Wilaya hiyo, katikati ni Mheshimiwa Spika na kulia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kongwa aliyemaliza muda wake Ndugu White Zuberi.Hafla hiyo imefanyika katika Ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa.

Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akikabidhi kompyuta kwa baadhi ya wakuu wa shule za sekondari za Wilaya ya Kongwa katika hafla ambayo ilihudhuriwa pia na baadhi ya viongozi wakiwemo Mkurugenzi wa Elimu TAMISEMI, Ndugu Julius Nestory, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kongwa aliyemaliza muda wake Ndugu White Zuberi na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Dkt. Omary Nkulo