WELCOME TO TANZANIA NATIONAL ASSEMBLY OFFICIAL BLOG: CONTACT US: P.O.BOX 941 DODOMA, TANZANIA, WEBSITE: parliament.go.tz , FIND US ON FACEBOOK >>> www.facebook.com/bungetz1, FOLLOW US ON TWITTER >>> @bunge_tz.>>>KARIBUNI

Thursday, March 21, 2024

WAJUMBE WA KAMATI YA LAAC WAMETEMBELEAA NA KUKAGUA MIRADI MIWILI KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA TARIME

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), Mheshimiwa Stansalaus Mabula akiambatana na wajumbe wa Kamati wakiangalia sehemu ya kunawia mikono nje ya bwalo la kulia chakula wakati kamati hiyo ilipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa shule mpya ya sekondari iliyopo Kijiji cha Nyasaricho katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime 

.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), Mheshimiwa Stansalaus Mabula akiangalia mchoro wa ramani ya Jengo la Halmashauri ya Wilaya ya Tarime wakati Kamati ilipotembelea na kukagua mradi huo.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), Mheshimiwa Stansalaus Mabula pomoja na Mjumbe wa Kamati Mheshimiwa Suma Fyandomo wakiangalia ujenzi wa maabara ya kemia kamati hiyo ilipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa shule mpya ya sekondari iliyopo Kijiji cha Nyasaricho katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime.

Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) wakiongozwa na Makamu Mwenyekiti Mheshimiwa Stansalaus Mabula wakikagua mradi wa la Jengo la Halmashauri ya Wilaya ya Tarime wakati Kamati ilipotembelea na kukagua mradi huo.

 

NAIBU SPIKA ZUNGU AFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA URUSI NCHINI


Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Mussa Azzan Zungu (Mb), akisalimiana na Balozi wa Urusi nchini, Mhe. Andrey Avetisyan alipomtembelea tarehe 20 Machi, 2024 katika ofisi ndogo za Bunge Jijini Dar es Salaam.



Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Mussa Azzan Zungu (Mb), akizungumza na Balozi wa Urusi nchini, Mhe. Andrey Avetisyan alipomtembelea tarehe 20 Machi, 2024 katika ofisi ndogo za Bunge Jijini Dar es Salaam.



Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Mussa Azzan Zungu (Mb), akimpatia zawadi Balozi wa Urusi nchini, Mhe. Andrey Avetisyan alipomtembelea tarehe 20 Machi, 2024 katika ofisi ndogo za Bunge Jijini Dar es Salaam.

KATIBU NENELWA AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA WAFANYAKAZI OFISI YA BUNGE












Katibu wa Bunge ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi ofisi ya Bunge, Ndg. Nenelwa Mwihambi, ndc akiongoza kikao cha Baraza hilo kilichofanyika tarehe 20 Machi, 2024 katika ofisi za Bunge Jijini Dodoma. 



 

Tuesday, March 19, 2024

KAMATI YA LAAC IMEKAGUA MIRADI MITATU KATIKA HALMASHAURI YA MJI WA GEITA

Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), Mheshimiwa Munde Tambwe akizungumza kwa niaba ya Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, wakati Kamati ilipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya katika zahanati ya Bulela iliyopo Halmashauri ya Mji wa Geita, kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati,Mheshimiwa Stansalaus Mabula na kushoto ni mjumbe wa Kamati hiyo Mheshimiwa Daimu Mpakate.



Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (LAAC),Mheshimiwa Stansalau Mabula akizungumza na watendaji mbalimbali wa Halmashauri ya Mji wa Geita wakati Kamati hiyo ilipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa Kituo cha Afya katika Zahanati ya Bulela iliyopo Manispaa ya Mji wa Geita

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (LAAC),Mheshimiwa Stansalau Mabula akiambatana na wajumbe wa Kamati hiyo wakikagua mradi wa ujenzi wa mpira wa miguu Geita katika Halmashauri ya Mji wa Geita.

 

 Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikalu (LAAC), wakiongozwa na Makamu mwenyekiti wa Kamati, Mheshimiwa Stansalaus Mabula wakonyeshwa mchoro wa ramani ya uwanja wa mpira wa miguu Geita wakati Kamati ilipotembelea na kukagua mradi huo.

 

Monday, March 18, 2024

KAMATI YA PAC YAKAGUA MRADI WA KUTOA MAJI ZIWA VIKTORIA NA KUSAMBAZA KATIKA MIJI YA TABOTA, IGUNGA NA NZEGA






















 

Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) imeridhishwa na utekelezaji wa mradi wa kupokea maji kutoka Ziwa Viktoria na kusambaza katika miji ya Tabora, Igunga na Nzega uliotekelezwa na Wizara ya Maji.

 

Kauli hiyo imetolewa na Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mheshimiwa Japhet Hasunga (Mb) wakati Kamati ilipotembelea na kukagua mradi huo na baadae kupokea taarifa ya utekelezaji wa mradi huo kwa awamu ya Kwanza na ya pili.

 

Alisema Kamati inaipongeza TUWASA kwa kusimamia vizuri mradi huo na kufikia malengo ya Serikali ya kufikisha maji safi na salama kwa wananchi katika maeneo mbalimbali ya ukanda wa ukame ambayo hayana vyanzo vya maji vya uhakika.

 

“TUWASA mmejitahidi sana, kwa macho tumejionea ubora wa miundombinu, sasa katika uendelevu wa mradi mlioueleza jitahidini na maeneo yaliyobakia ya Sikonge, Urambo Isikizya, kaliua, Shelui na Tinde maji yawafikie wananchi.” Alisema

 

Mheshimiwa Hasunga aliwasisitiza TUWASA kuhakikisha wanaongeza umakini na usimamizi wa miundombinu ya mradi huo kwa lengo la kuondoa kabisa changamoto ya upotevu wa maji ili wananchi wengi zaidi waweze kunufaika na mradi huo.

 

“Kwenye changamoto ya upotevu wa maji tutaendelea kupambana, ongezeni usimamizi ili maji yasipotee yawafikie wananchi.” Alisema

 

Mapema akiwasilisha taarifa ya Mradi huo Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Tabora (TUWASA) Mhandisi Mayunga Kashilimu amesema kukamilika kwa mradi huo kumewezesha wananchi zaidi ya milioni moja na laki mbili (1,200,000) wanapata huduma ya maji safi na salama.

 

“upatikanaji wa maji safi na salama umeongezeka hadi kufikia asilimia 100 katika Manispaa ya Tabora na miji ya Igunga, Nzega, Makao makuu ya Wilaya ya uyui pamoja na vijiji 102

 

Alisema  huduma bora ya Maji inachangia kuboresha afya za wananchi wa maeneo husika na kuinua uchumi kupitia maendeleo ya sekta zingine zinazotegemea maji kama vile viwanda.

 

Kamati ya PAC, kesho inatarajia kukagua mradi wa kiwanda cha kupaka rangi mabomba kwa ajili ya kuweka mfumo wa upashaji joto mabomba katika  mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP), Wilaya ya Kahama, Mkoani Shinyanga

 

 Mwisho

KAMATI YA LAAC IMEKAGUA UJENZI WA HOSPITALI YA HALMASHAURI YA MANISPAA YA BUKOBA MKOANI KAGERA



Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (LAAC), wakiongozwa na Makamu Mwenyekiti Mheshimiwa Stansalus Mabula, wakiangalia msingi wa mojawapo ya jengo la Hospitali ya Manispaa ya Bukoba wakati Kamati hiyo potembelea na kukagua ujenzi wa  hospitali hiyo katika Mkoa wa Kagera

Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (LAAC), wakiongozwa na Makamu Mwenyekiti Mheshimiwa Stansalus Mabula, wakikagua mradi wa ujenzi wa Hospitali ya  Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba wakati Kamati hiyo ilipotembelea na kukagua mradi huo.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (LAAC), akieleza jambo mbele ya watendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba wakati Kamati hiyo ilipotembelea na kukagua ujenzi wa  Hospitali ya Manispaa hiyo katika Mkoa wa Kagera. 

Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (LAAC), wakiongozwa na Makamu Mwenyekiti Mheshimiwa Stansalus Mabula, wakiangalia msingi wa mojawapo ya jengo la Hospitali ya Manispaa ya Bukoba wakati Kamati hiyo potembelea na kukagua ujenzi wa  hospitali hiyo katika Mkoa wa Kagera. 






 

Sunday, March 17, 2024

KAMATI YA LAAC YATEMBELEA HOSPITALI YA HALMASHAURI YA WILAYA YA MISENYI NA SHULE YA SEKONDARI KITOBO KATIKA HALMASHAURI HIYO

Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (LAAC), wakiongozwa na Makamu Mwenyekiti Mheshimiwa Stansalus Mabula, wakikagua ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Misenyi mkoani Kagera.

Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (LAAC), wakiongozwa na Makamu Mwenyekiti Mheshimiwa Stansalus Mabula, wakikagua ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Misenyi mkoani Kagera.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (LAAC), akieleza jambo mbele ya watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misenyi wakati Kamati hiyo ilipotembelea na kukagua ujenzi wa  Hospitali ya Halmashauri hiyo.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (LAAC), pamoja na wajumbe wa Kamati hiyo wakiangalia mashine ya mionzi (x-rays) wakati Kamati hiyo ilipotembelea na kukagua ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Misenyi. 



 Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (LAAC), akizungumza wakati Kamati hiyo ilipotembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari Kitobo   iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Misenyi.