WELCOME TO TANZANIA NATIONAL ASSEMBLY OFFICIAL BLOG: CONTACT US: P.O.BOX 941 DODOMA, TANZANIA, WEBSITE: parliament.go.tz , FIND US ON FACEBOOK >>> www.facebook.com/bungetz1, FOLLOW US ON TWITTER >>> @bunge_tz.>>>KARIBUNI

Wednesday, August 23, 2017

WAJUMBE WA CPA TAWI LA TANZANIA WAKUTANA NA WAJUMBE WA CPA TAWI LA CANADA JIJINI DAR ES SALAAM

 Mwenyekiti wa Kamati Tendaji ya  Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Tawi la Tanzania Dkt Raphael Chegeni (katikati) akiongoza kikao wakati Wajumbe wa Kamati hiyo walipokutana na Wajumbe wa Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Tawi la Canada  katika Ofisi Ndogo za Bunge Jijini Dar es Salaam mapema leo.

Mwenyekiti  wa Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Tawi la Canada  Mhe. Yasmin Ratansi (wa kwanza kushoto) akisisitiza jambo wakati Wajumbe wa Chama hicho kutoka Canada walipokutana na Wajumbe wa Kamati Tendaji ya  Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Tawi la Tanzania katika Ofisi Ndogo za Bunge Jijini Dar es Salaam mapema leo

Mwenyekiti wa Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Tawi la Canada ambae pia ni Mbunge, Mhe. Yasmin Ratansi akimkabidhi  zawadi Mwenyekiti wa Kamati Tendaji ya  Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Tawi la Tanzania Dkt Raphael Chegeni mara baada ya Wajumbe wa pande zote mbili kuzungumza mapema leo katika Ofisi Ndogo za Bunge Jijini Dar es Salaam.


Wajumbe wa Kamati Tendaji ya  Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Tawi la Tanzania katika picha ya pamoja na Wajumbe wa   Chama cha Mabunge ya Jumuiya ya Madola Tawi la Canada mara baada ya mazungumzo katika Ofisi Ndogo za Bunge Jijini Dar es Salaam

Monday, August 7, 2017

MHE. SPIKA AMTEMBELEA RAIS WA IRANI

Spika wa Bunge Mheshimiwa Job Ndugai ametembelea Ikulu ya Irani na kufanya mazungumzo na Rais wa Iran, Mheshimiwa Hassan Rouhani ambapo Mheshimiwa Spika amempongeza kuteuliwa kwake kwa mara ya pili na kumuahidi ushirikiano wa karibu baina ya Bunge la Tanzania na lile la Iran. Mheshimiwa Spika alikuwa miongoni mwa wageni mashuhuri walioalikwa kushuhudia kuapishwa kwa Rais Rouhani katika sherehe zilizofanyika kwenye Bunge la Iran Mjini Tehran.

Spika wa Bunge Mheshimiwa Job Ndugai ametembelea Ikulu ya Irani na kufanya mazungumzo na Rais wa Iran, Mheshimiwa Hassan Rouhani ambapo Mheshimiwa Spika amempongeza kuteuliwa kwake kwa mara ya pili na kumuahidi ushirikiano wa karibu baina ya Bunge la Tanzania na lile la Iran. Mheshimiwa Spika alikuwa miongoni mwa wageni mashuhuri walioalikwa kushuhudia kuapishwa kwa Rais Rouhani katika sherehe zilizofanyika kwenye Bunge la Iran Mjini Tehran. 
Mheshimiwa Spika akiwa na mwenyeji wake


Friday, August 4, 2017

MHE. NDUGAI AKUTANA NA SPIKA WA BUNGE LA IRAN NA KUFANYA NAE MAZUNGUMZO

Mhe. Spika Job Ndugai  leo amekutana na Spika wa Bunge  la Iran, Mhe. Dkt. Ali  Larijani na kufanya nae mazungumzo yenye lengo la kuimarisha mahusiano ya kibunge baina ya Bunge la Tanzania na Iran.

Mhe. Spika Job Ndugai  leo amekutana na Spika wa Bunge  la Iran, Mhe. Dkt. Ali  Larijani na kufanya nae mazungumzo yenye lengo la kuimarisha mahusiano ya kibunge baina ya Bunge la Tanzania na Iran.

Mhe. Spika Job Ndugai  akisalimiana na mwenyeji wake

UAMUZI WA SPIKA KUHUSU WABUNGE WAWILI WA CUF WALIOFUKUZWA UANACHAMA



Thursday, August 3, 2017

MHE.SPIKA AWASILI TEHRAN KUSHUHUDIA KUAPISHWA KWA RAIS WA IRAN

Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akiwasili Tehran kushiriki hafla ya kuapishwa kwa Rais wa 12 wa Iran ambapo kwa mujibu wa Katiba ya nchi hiyo, Rais huapishwa Bungeni na Spika.Mheshimiwa Spika yuko Tehran kwa mwaliko wa Spika wa Bunge la nchi hiyo akiwawakilisha Maspika wa Afrika

 

Mhe. Spika Job Ndugai akizungumza  na Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma za Jamii katika Bunge la Iran, Mhe Dkt, Abdolreza Aziz,wakati alipotembelea Bungeni hapo kuhudhuria hafla ya kuapishwa kwa Rais wa 12 wa Iran.


Wednesday, August 2, 2017

MHE. SPIKA ATEMBELEA BUNGE LA UMOJA WA FALME ZA KIARABU

 Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai ametembelela Bunge la Umoja wa Falme za Kiarabu lililopo Abu Dhabi na kufanya mazungumzo  na Spika wa Bunge hilo, Mhe. Dkt. Amal Al Qubaisi ambapo amewasilisha  mapendekezo rasmi ya kuanzisha umoja na urafiki wa kibunge baina ya Bunge la Tanzania na Bunge la Umoja wa Falme za Kiarabu.Mapendekezo hayo yamekubaliwa

Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akisalimiana na Spika wa Bunge la Umoja wa Falme za Kiarabu, Mhe. Dkt. Amal Al Qubaisi baada ya kutembelea Bunge hilo na kufanya nae mazungumzo ambapo pia amewasilisha  mapendekezo rasmi ya kuanzisha umoja na urafiki wa kibunge baina ya Bunge la Tanzania na Bunge la Umoja wa Falme za Kiarabu


Mhe. Spika Job Ndugai akikasaini kitabu cha wageni wakati alipotembelea Bunge la Umoja wa Falme za Kiarabu  huku akiangaliwa na Spika wa Bunge hilo, Mh. Dkt. Amal Al Qubaisi (katikati) na Katibu wa Bunge Ndg. Ahmed Shabeeb
Mhe. Spika Job Ndugai akikabidhi ujumbe wake maalum kwa  Spika wa Bunge la Umoja wa Falme za Kiarabu, Mh. Dkt. Amal Al Qubaisi.


Mhe. Spika Job Ndugai akipewa maelezo kutoka kwa  Spika wa Bunge la Umoja wa Falme za Kiarabu, Mhr. Dkt. Amal Al Qubaisi wakati alipotembelea Bunge hilo .