WELCOME TO TANZANIA NATIONAL ASSEMBLY OFFICIAL BLOG: CONTACT US: P.O.BOX 941 DODOMA, TANZANIA, WEBSITE: parliament.go.tz , FIND US ON FACEBOOK >>> www.facebook.com/bungetz1, FOLLOW US ON TWITTER >>> @bunge_tz.>>>KARIBUNI

Thursday, June 22, 2017

TAASISI YA ISLAMIC FOUNDATION YAFUTURISHA WABUNGE

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mheshimiwa Mwigulu Nchemba akipata futari iliyoandaliwa na Taasisi ya Islamic Foundation (TIF) kwa ajili wa Waheshimiwa Wabunge, Wafanyakazi wa Bunge na wageni wengine. Katikakati ni Mwenyekiti wa Taasisi hiyo, Sheikh Aref Mubark Nahad na kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Mkuranga Mheshimiwa Abdallah Ulega.Hafla hiyo ilifanyika katika Viwanja vya Bunge Mjini Dodoma Juni 21, 2017.

Waheshimiwa Wabunge wakipata futari iliyoandaliwa na Taasisi ya Islamic Foundation (TIF) kwa ajili wa Waheshimiwa Wabunge, Wafanyakazi wa Bunge na wageni wengine katika Viwanja vya Bunge Mjini Dodoma.

Waandishi wa Habari za Bunge wakihudhuria katika futari iliyoandaliwa na Taasisi ya Islamic Foundation (TIF) kwa ajili wa Waheshimiwa Wabunge, Wafanyakazi wa Bunge na wageni wengine katika Viwanja vya Bunge Mjini Dodoma.

Mbunge wa Jimbo la Mkuranga, Mheshimiwa Abdallah Ulega akizungumza mara baada ya kumaliza kufuturu, kulia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Islamic Foundation (TIF), Sheikh Mohamed Issa na kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi wa Vyombo vya Habari vya Taasisi hiyo, Sheikh Mohamed Issa.

Wednesday, June 21, 2017

SPIKA AFUTURISHA WABUNGE, WAFANYAKAZI NA WAZEE WA DODOMA

Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai akibadilishana mawazo na Waziri wa Elimu, Teknolojia, Sayansi na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako wakati wa futari iliyoandaliwa na Spika kwa ajili ya wabunge, wafanyakazi wa Bunge na Wazee wa Mkoa wa Dodoma

 Mheshimiwa Spika Job Ndugai akizungumza na baadhi ya wabunge walioshiriki katika futari aliyoaindaa


Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai akifurahia jambo akiwa na Waziri Mkuu, Mhesmiwa Kassim Majaliwa wakati wa Futari katika Viwanja vya Bunge, Mjini Dodoma.

Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai akiagana na Waziri Mkuu, Mheshimiwa Kassim Majaliwa mara baada ya Waziri Mkuu kushiriki katika Futari iliyoandaliwa na Spika katika Viwanja vya Bunge Mjini Dodoma.

Tuesday, June 20, 2017

Spika wa Bunge, amekutana na uongozi wa Chama cha Askari Wastaafu wa Vita ya Pili ya Dunia (TLC) ofisini kwake Mjini Dodoma

Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai leo amekutana na uongozi wa Chama cha Askari Wastaafu wa Vita ya Pili ya Dunia (TLC) ofisini kwake Mjini Dodoma

Afisa Utawala wa Chama cha Wastaafu wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia (TLC), Ndugu Charles Lubala akieleza lengo la ujumbe huo mbele ya Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai.


Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai akizungumza na wazee hao askari wastaafu.
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai akipokea barua kutoka kwa Mwenyekiti wa Chama hicho, Ndugu Rashid Bakari Ngonja inayowatambulisha pamoja kuomba mchango kwa ajili ya kukiwezesha chama kufanya mkutano mkuu wake.

Mheshimiwa Spika, Job Ndugai akiagana na wageni hao

SPIKA NDUGAI APATA UGENI KUTOKA BUNGE LA MSUMBIJI LEO OFISINI KWAKE MJINI DODOMA

 Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) akimsikiliza Kiongozi wa Msafara na Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kutoka Bunge la Msumbiji, Mhe. Lucas Jeremias (katikati) pale ugeni kutoka kamati ya kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kutoka Bunge la Msumbiji ulipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma
Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) akimsikiliza Kiongozi wa Msafara na Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kutoka Bunge la Msumbiji, Mhe. Lucas Jeremias (katikati) pale ugeni kutoka kamati ya kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kutoka Bunge la Msumbiji ulipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma, kulia ni Mjumbe wa kamati hiyo Mhe. Beatriz Chaguala.

Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) akisisitiza jambo mbele ya kamati ya kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kutoka Bunge la Msumbiji uliomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma, katikati ni Kiongozi wa Msafara na Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kutoka Bunge la Msumbiji, Mhe. Lucas Jeremias na kulia ni Mjumbe wa kamati hiyo Mhe. Beatriz Chagula.



Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) akizungumza  mbele ya kamati ya kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kutoka Bunge la Msumbiji ulipomtembelea leo Ofisini kwake Mjini Dodoma, wa pili kushoto ni Kiongozi wa Msafara na Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kutoka Bunge la Msumbiji, Mhe. Lucas Jeremias

Sunday, June 18, 2017

SPIKA NDUGAI AONGOZA WABUNGE KATIKA HARAMBEE YA UJENZI WA JENGO LA JUMUIYA YA KIKRISTO TANZANIA TUKIO LILILOFANYIKA LEO MJINI DODOMA

Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai akizungumza wakati wa  harambee kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Jumuiya ya kikristo Tanzania, tukio lililofanyika leo Mjini Dodoma. Kushoto ni  Waziri Mkuu Mstaafu, Mheshimiwa Mizengo Pinda  na katikati ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya kikristo Tanzania, Askofu Dkt. Alex Malasusa



Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kulia) akisalimiana na Waziri Mkuu Mstaafu, Mheshimiwa Mizengo Pinda (kushoto) kabla ya kuanza harambee kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Jumuiya ya kikristo Tanzania, katika tukio lililofanyika leo Mjini Dodoma. katikati ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya kikristo Tanzania, Askofu Dkt. Alex Malasusa


Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (wa pili kulia)akiongoza Wabunge Mbali mbali kucheza nyimbo ya injili kama njia moja wapo ya kuhamasisha uchangiaji kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Jumuiya ya kikristo Tanzania, tukio lililofanyika leo Mjini Dodoma



Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai (kushoto) akiteta jambo na Katibu wa Bunge, Dkt. Thomas Kashililah (kulia) baada ya kumalizika kwa harambee kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Jumuiya ya kikristo Tanzania, tukio lililofanyika leo Mjini Dodoma, Pia Spika Ndugai aliongoza Wabunge katika harambee hiyo.



Waziri Mkuu Mstaafu, Mheshimiwa Mizengo Pinda (wa pili kushoto) akizungumza jambo baada ya kumalizika kwa harambee kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Jumuiya ya kikristo Tanzania, kulia ni Katibu wa Bunge, Dkt. Thomas Kashililah, kushoto ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya kikristo Tanzania, Askofu Dkt. Alex Malasusa na wa pili kulia ni Ndg. Elton Mapesa.



Waziri Mkuu Mstaafu, Mheshimiwa Mizengo Pinda (kushoto) akiagana na Katibu wa Bunge, Dkt. Thomas Kashililah (kulia) baada ya kumalizika kwa harambee kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Jumuiya ya kikristo Tanzania. Katika harambee hiyo, Spika wa Bunge, Mheshimiwa Job Ndugai aliwaongoza wa Bunge katika uchangiaji wa ujenzi wa jengo hilo.